KLABU ya Arsenal
itafikiria ofa iliyoimarishwa kutoka Inter Milan kwa ajili ya kumsajili
mshambuliaji wa kimataifa wa Ujerumani Lukas Podolski. Podolski mwenye
umri wa miaka 29 ameshindwa kupata namba katika kikosi cha kwanza cha
Arsenal msimu huu huku akiukosa mchezo dhidi ya Southampton jana
kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya nyonga. Meneja wa klabu hiyo
Arsene Wenger amesema ofa ya kwanza waliyotoa Inter ilikuwa ndogo hivyo
kama wakirudi tena na fungu la kueleweka wataangalia uwezekano wa
kufanya biashara. Podolski alinunuliwa na Arsenal kwa kitita cha paundi
milioni 11 akitokea klabu ya Cologne mwaka 2012 lakini amefanikiwa
kuanza kucheza mechi 39 pekee katika akiwa chini ya Wenger. Mshambuliaji
huyo amefunga jumla ya mabao 31 katika mechi 82 alizoichezea Arsenal
katika mashindano yote.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Ijumaa, 2 Januari 2015
ARSENAL KUISIKILIZA INTER KAMA WAKIONGEZA OFA YA KUMTAKA PODOLSKI.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni