STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Ijumaa, 2 Januari 2015

ARSENAL KUISIKILIZA INTER KAMA WAKIONGEZA OFA YA KUMTAKA PODOLSKI.


KLABU ya Arsenal itafikiria ofa iliyoimarishwa kutoka Inter Milan kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Ujerumani Lukas Podolski. Podolski mwenye umri wa miaka 29 ameshindwa kupata namba katika kikosi cha kwanza cha Arsenal msimu huu huku akiukosa mchezo dhidi ya Southampton jana kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya nyonga. Meneja wa klabu hiyo Arsene Wenger amesema ofa ya kwanza waliyotoa Inter ilikuwa ndogo hivyo kama wakirudi tena na fungu la kueleweka wataangalia uwezekano wa kufanya biashara. Podolski alinunuliwa na Arsenal kwa kitita cha paundi milioni 11 akitokea klabu ya Cologne mwaka 2012 lakini amefanikiwa kuanza kucheza mechi 39 pekee katika akiwa chini ya Wenger. Mshambuliaji huyo amefunga jumla ya mabao 31 katika mechi 82 alizoichezea Arsenal katika mashindano yote.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox