STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Ijumaa, 2 Januari 2015

KAMA KAWAIDA YAKE MOURINHO ALIA NA WAAMUZI BAADA YA KICHAPO CHA 5-3 KUTOKA KWA SPURS.

MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho anaamini kikosi chake kingeweza kuichapa Tottenham Hotspurs kama wangezawadiwa penati ambayo ingewafanya kuongoza katika mchezo huo. Baada ya Diego Costa kuifungiwa Chelsea bao la kuongoza, timu hiyo ilinyimwa penati na mwamuzi Phil Dowd wakati Jan Vertonghen aliposhika mpira katika eneo la hatari, na baadae kuja kupoteza mchezo huo kwa kufungwa mabao 5-3. Mourinho alimlaumu mwamuzi wa mchezo huo kwa kushindwa kutoa penati hiyo kwani ingewapa nafasi nzuri ya kushinda mchezo huo. Hata hivyo baadhi wachambuzi wa soka wameshindwa kukubaliana na Mourinho wakidai kuwa haikustahili kuwa penati hivyo mwamuzi alikuwa sahihi. Chelsea ambao walikuwa wakiongoza kwa tofauti ya alama nane katika msimamo wa Ligi Kuu Novemba mwaka jana sasa wako juu ya Manchester City kutokana na mpangilio wa herufi kufuatia kipigo hicho cha jana.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox