STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 8 Januari 2015

KESSY AGOMA KUPEWA ZAWADI YA MCHEZAJI BORA ZANZIBAR

3
Mchezaji bora wa mechi, Kessy (kulia) 

HASSAN Ramadhan Kessy aliyechaguliwa kuwa mchezaji bora Simba ikitinga nusu fainali ya kombe la Mapinduzi kwa kuifunga mabao 4-0 Taifa ya Jang’ombe katika kipute cha robo fainali kilichofanyika uwanja wa Amaan jana usiku ameigomea zawadi hiyo.
Akizungumza jana dakika chache baada ya mechi kumalizika,  Kessy alimshukuru Mungu kwa kucheza vizuri na kuchaguliwa kuwa mchezaji bora wa mechi na kupewa zawadi ya King’amuzi cha Azam TV.
Hata hivyo beki huyo wa kulia aligoma kupewa hadhi ya kuwa mchezaji bora badala yake alisema mfungaji wa mabao matatu katika ushindi wa Simba, Ibrahim Hajibu ‘Mido’ ndiye alistahili kuwa mchezaji bora.
“Nimepewa zawadi, nashukuru. Lakini sijui wametumia vigezo gani, mimi naona Hajibu (Ibrahim) alistahili kuwa mchezaji bora”. Alisema Kessy.
Nyota huyo aliyejiunga na Simba wakati wa dirisha dogo la usajili desemba mwaka jana akitokea Mtibwa Sugar alisema kikosi cha Simba kinazidi kuimarika chini ya kocha mpya.
“Tunashukuru Mungu tunacheza vizuri. Kocha amekuja na mbinu mpya. Mashabiki ‘waisapoti’ timu yao. Simba ni timu yetu sote, tukiwa na umoja tutafanya vizuri”. Alisisitiza Kessy.
Dakika za lala salama katika mechi hiyo, Kessy alitolewa na nafasi yake ilichukuliwa na beki mkongwe, Masoud Nassor ‘Cholo’.
Simba inasubiri mpinzani wake wa nusu fainali katika mechi ya mapema leo saa 9:00 alasiri baina ya mabingwa watetezi wa kombe hilo, KCC ya Uganda na Polisi Zanzibar.

Mechi nyingine ya robo fainali itaanza majira ya saa 11:00 jioni baina ya Azam fc na Mtibwa Sugar, wakati saa 2:15 usiku katika uwanja  huo wa Amaan, Yanga watahitimisha hatua hiyo kwa kuchuana na JKU ya Zanzibar.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox