KATIKA tetesi za usajili
klabu ya Chelsea inajiandaa kutenga kitita cha paundi milioni 200 kwa
ajili ya kutengua mkataba na kumsajili mshambuliaji wa Barcelona Lionel
Messi. Katika siku za karibuni kumekuwa na tetesi kutoka vyombo vya
habari nchini Hispania kuwa Messi hana furaha Barcelona toka Luis
Enrique ateuliwe kuwa kocha, ingawa habari hizo zimepingwa vikali na
rais wake aliyedai mchezaji huyo ana furaha na hataondoka. Kwa upande
mwingine Liverpool nao wanataka kumsajili beki wa kimataifa wa Uingereza
na klabu ya Manchester City James Milner mwenye umri wa miaka 29 ambaye
mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu huu. Gazeti la Daily Stars
nalo limeripoti kuwa Manchester United wametoa ofa kwa ajili ya beki wa
kati wa kimataifa wa Ujerumani Mats Hummels pamoja na klabu yake ya
Borussia Dortmund kuweka ngumu kuwa haitamuuza beki huyo. Winga mahiri
wa kimataifa wa Uingereza Andros Townsend mwenye umri wa miaka 23
amesisitiza kuwa anataka kuendelea kubakia Tottenham Hotspurs kwa
kipindi kirefu kijacho pamoja na kuhusishwa na tetesi za kuondoka. Klabu
ya Arsenal wametupiwa ofa yao ya paundi milioni tano na klabu ya Dinamo
Zagreb kwa ajili ya kumsajili kiungo Marcelo Brozovic. Klabu za
Everton, Liverpool, Tottenham Hotspurs na Valencia nazo zinaonekana
kumfukuzia nyota huyo mwenye umri wa miaka 22.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Alhamisi, 8 Januari 2015
Home
/
Unlabelled
/
TETESI ZA USAJILI ULAYA: CHELSEA WAKO TAYARI KUMTENGEA PAUNDI MILIONI 200 MESSI, LIVERPOOL WAMTAKA MILNER, MAN UNITED WAMKOMALIA HUMMELS.
TETESI ZA USAJILI ULAYA: CHELSEA WAKO TAYARI KUMTENGEA PAUNDI MILIONI 200 MESSI, LIVERPOOL WAMTAKA MILNER, MAN UNITED WAMKOMALIA HUMMELS.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni