MCHEZAJI nyota wa klabu
ya Paris Saint-Germain-PSG, Javier Pastore amesema timu hiyo iko tayari
kumsajili Lionel Messi kama mshambuliaji huyo wa Barcelona atawekwa
sokoni na kudai kuwa pesa haitakuwa tatizo. Messi amekuwa na uhusiano wa
kuyumbayumba na klabu hiyo msimu huu jambo ambalo limezua maswali
kuhusiana na mustakabali wake huku tetesi hizo zikiongezeka baada ya
kuondoka kwa wakurugenzi wa michezo Andoni Zubizarreta na Carles Puyol
wiki hii. Messi mwenyewe alikaririwa mapema msimu huu akidai kuwa
pengine anaweza kuondoka Barcelona katika siku za usoni na Pastore
anaamini kuwa PSG itakuwa tayari kumsajili nyota huyo pindi nafasi
itakapotokea. Pastore amesema kama itatokea Messi kuondoka Barcelona
anadhani mmiliki wa PSG atakuwepo kujaribu kumsajili mchezaji huyo kwani
pesa sio tatizo kutokana na rasilimali zilizopo katika klabu
hiyo. Messi ana mkataba na Barcelona mbao unaishia katika majira ya
kiangazi mwaka 2018 lakini kama itatokea kuondoka klabu itakayotaka
kumsajili italazimika kutoa kitita cha euro milioni 250.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Alhamisi, 8 Januari 2015
PSG INAWEZA KUMSAJILI MESSI - PASTORE.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni