KATIKA habari za tetesi
za usajili meneja wa klabu ya Bayern Munich Pep Guardiola anajipanga
kuongeza nguvu katika nafasi ya ulinzi wa kati katika kikosi chake na
tayari ameshamuweka Raphael Varane katika rada zake. Taarifa zinadai
kuwa tayari Guardiola ameshazungumza na wakala wa mchezaji huyo Jorge
Mendes juu ya uwezekano wa kumsajili kwa kitita cha euro milioni
40. Baada ya klabu ya Juventus kushindwa beki kwa kiungo wa Galatasaray
Wesley Sneijder, timu hiyo sasa imeamua kuhamishia nguvu zake kwa
mshambuliaji wa Manchester United Adnan Januzaj. Tukibaki hapohapo
nchini Italia, klabu ya Inter Milan imemtengea kitita cha paundi milioni
saba kiungo wa Liverpool Lucas Leiva. Hata hivyo taarifa zinadai kuwa
Brendan Rodgers ametupilia mbali ofa hiyo akidai kuwa ndogo sana kwa
ajili ya kiungo huyo mwenye umri wa miaka 28. Naye mshambuliaji wa klabu
ya Arsenal, Yaya Sanogo amekataa ofa kutoka klabu za Ufaransa ili aweze
kubakia katika Ligi Kuu na anatarajiwa kujiunga na klabu ya Crystal
Palace kwa mkopo. Klabu ya Tottenham Hotspurs imehusishwa na tetesi za
kumuwinda kiungo wa klabu ya Juventus Sebastian Giovinco ambaye mkataba
wake unamalizika Juni mwaka huu. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 27
amekataa kusaini mkataba mpya na mabingwa hao wa Serie A. Klabu ya Real
Madrid imepiga hatua kwa kutenga kitita cha paundi milioni 30 kwa ajili
ya golikipa wa Manchester United David de Gea. Hata hivyo dili hilo
linaweza kushindikana kwani United wamepania kumuongeza mkataba mwingine
mnono golikipa huyo ili waweze kumshawishi kubakia Old Trafford.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumamosi, 10 Januari 2015
Home
/
Unlabelled
/
TETESI ZA USAJILI ULAYA: GUARDIOLA AMTENGEA VARANE PAUNDI MILIONI 40, JUVENTUS SASA WAHAMIA KWA JANUZAJ, MADRID WAANZA KUMSARANDIA DE GEA.
TETESI ZA USAJILI ULAYA: GUARDIOLA AMTENGEA VARANE PAUNDI MILIONI 40, JUVENTUS SASA WAHAMIA KWA JANUZAJ, MADRID WAANZA KUMSARANDIA DE GEA.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni