STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumamosi, 10 Januari 2015

TETESI ZA USAJILI ULAYA: GUARDIOLA AMTENGEA VARANE PAUNDI MILIONI 40, JUVENTUS SASA WAHAMIA KWA JANUZAJ, MADRID WAANZA KUMSARANDIA DE GEA.

KATIKA habari za tetesi za usajili meneja wa klabu ya Bayern Munich Pep Guardiola anajipanga kuongeza nguvu katika nafasi ya ulinzi wa kati katika kikosi chake na tayari ameshamuweka Raphael Varane katika rada zake. Taarifa zinadai kuwa tayari Guardiola ameshazungumza na wakala wa mchezaji huyo Jorge Mendes juu ya uwezekano wa kumsajili kwa kitita cha euro milioni 40. Baada ya klabu ya Juventus kushindwa beki kwa kiungo wa Galatasaray Wesley Sneijder, timu hiyo sasa imeamua kuhamishia nguvu zake kwa mshambuliaji wa Manchester United Adnan Januzaj. Tukibaki hapohapo nchini Italia, klabu ya Inter Milan imemtengea kitita cha paundi milioni saba kiungo wa Liverpool Lucas Leiva. Hata hivyo taarifa zinadai kuwa Brendan Rodgers ametupilia mbali ofa hiyo akidai kuwa ndogo sana kwa ajili ya kiungo huyo mwenye umri wa miaka 28. Naye mshambuliaji wa klabu ya Arsenal, Yaya Sanogo amekataa ofa kutoka klabu za Ufaransa ili aweze kubakia katika Ligi Kuu na anatarajiwa kujiunga na klabu ya Crystal Palace kwa mkopo. Klabu ya Tottenham Hotspurs imehusishwa na tetesi za kumuwinda kiungo wa klabu ya Juventus Sebastian Giovinco ambaye mkataba wake unamalizika Juni mwaka huu. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 27 amekataa kusaini mkataba mpya na mabingwa hao wa Serie A. Klabu ya Real Madrid imepiga hatua kwa kutenga kitita cha paundi milioni 30 kwa ajili ya golikipa wa Manchester United David de Gea. Hata hivyo dili hilo linaweza kushindikana kwani United wamepania kumuongeza mkataba mwingine mnono golikipa huyo ili waweze kumshawishi kubakia Old Trafford.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox