Manchester
United imeripotiwa imepiga hatua nyingine katika mbio zake za kumnyakua
winga Gareth Bale baada ya Real Madrid kuonekana kukubali ofa yao kwa
mchezaji huyo.
United wanaiwania kwa udi na uvumba saini ya Bale baada ya msimu
kumalizika, kikosi hicho cha Louis van Gaal kikihitaji mchezaji mwenye
kiwango cha juu.
Imeripotiwa kuwa kiasi cha pauni milioni 150 kimeandaliwa kwa ajili
usajili huo, huku ripoti zaidi zikieleza jana kuwa Madrid sasa
wameonekana kukubali ofa hiyo.
Madrid watafanya biashara hiyo kama ofa hiyo itawafikia na wameripoti
kuwa tayari wameshaanza kusaka mbadala wake, wakimtaka mchezaji wa
Borussia Dortmund, Marco Reus.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni