TETESI za usajili
zinaoendelea kupamba vichwa vya habari ulimwenguni kwa leo ni klabu ya
Real Madrid kutaka kumuongeza mkataba winga wake mahiri Gareth Bale. Kwa
mujibu wa taarifa zilizotolewa na gazeti la Daily Star, Bale
anatarajiwa kuongezwa mkataba ambao utamuweka Santiago Bernabeu mpaka
mwaka 2021. Baada ya kutangaza kuondoka Liverpool mwishoni mwa msimu huu
Steven Gerard mwenye umri wa miaka 34 sasa amekuwa akiwindwa na vilabu
mbalimbali mojawapo ikiwa ni Los Angeles Galaxy ya Marekani ambayo
imepanga kumtengea kitita cha paundi milioni 20. Klabu hiyo imepanga
kumlipa Gerrard mshahara wa paundi 100,000 kwa wiki huku wakimpatia
mkataba wa miaka minne kuitumikia timu hiyo. Beki mahiri wa klabu ya
Borussia Dortmund Mats Hummels yuko tayari kuondoka katika timu hiyo
lakini bado hajaamua kama anataka kwenda Manchester United au
Arsenal. Endapo kama klabu hizo zitamuhitaji zitalazimika kutoa kitita
cha cha kufikia euro milioni 50 kwa ajili ya saini ya beki huyo ambaye
amekuwa na msimu usioridhisha Dortmund. Kocha wa zamani wa Manchester
United David Moyes amepania kuwasajili Mohamed Salah na Arouna Kone
katika klabu yake ya Real Sociedad katika kipindi hiki cha
usajili. Moyes amepanga kuwachukua wachezaji wote hao wawili kwa mkopo
ikiwa ni sehemu ya kuimarisha kikosi chake ili kiepuke hatari ya kushuka
daraja.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumapili, 4 Januari 2015
Home
/
Unlabelled
/
TETESI ZA USAJILI ULAYA: MADRID KUMUONGEZA MKATABA BALE, LA GALAXY YAMTENGEA MSHAHARA MNONO GERRARD.
TETESI ZA USAJILI ULAYA: MADRID KUMUONGEZA MKATABA BALE, LA GALAXY YAMTENGEA MSHAHARA MNONO GERRARD.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni