Nahodha wa Chelsea,
John Terry amesaini mkataba mpya na klabu yake ambao utamuwezesha kulamba pauni
150,000 kwa wiki.
Mkataba huo
mpya wa Terry mwenye umri wa miaka 34 na Chelsea utamalizika mwishoni mwa msimu
huu wa 2015-16.
Kocha Mkuu wa
Chelsea, Jose Mourinho ameutaja mkataba huo kuwa ni sahihi na kusisitiza si
asante kwa Terry, badala yake ni kutokana na uwezo anaopuonyesha.
Terry ameichezea
Chelsea mechi 661 tokea mwaka 1998 alipocheza mechi yake ya kwanza kabla ya
kupata namba ya uhakika katika kikosi cha kwanza mwaka 2000.
Beki huyo anaendelea kushikilia rekodi ya beki aliyefunga mabao mengi zaidi akiwa na Chelsea baada ya kupachika 64.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni