STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatatu, 4 Aprili 2016

BILIONEA AWA MWENYEKITI MTENDAJI WA KLABU YA VPL..................

Dr-Sulaiman-Al-Fahim-Port-001


Mfanyabiashara maarufu wa kiarabu Dk Sulaiman Al-Fahim ametangazwa kuwa mwenyekiti mtendaji wa klabu ya African Lyon ambayo itashiriki ligi kuu ya Tanzania Bara msimu ujao.

Mmiliki wa klabu ya African Lyon, Rahim Kangezi alisema kuwa waliamua kumuomba Al Fahim kushika nafasi hiyo kutokana na uzoefu wake katika michezo hasa mpira wa miguu mbali ya kuwa mfanyabiashara bilionea katika nchi za Uarabuni na duniani kwa ujumla.

Kangezi alisema kuwa Al Fahim ni Rais wa kampuni ya Arab Union for Real Estate Development ya Dubai na miaka ya nyuma alikuwa msemaji wa kampuni inayomiliki klabu tajiri duniani, Manchester City, Abu Dhabi United Group (ADUG). ADUG iliinunua Manchester City Septemba, 2008.

Pia Al Fahim alitaka kununua klabu ya Portsmouth ambayo ilikuwa inashiriki ligi kuu ya Uingereza, lakini mpango huo haukuweza kukamilika.

Kangezi alisema kuwa Al Fahim ataanza kazi rasmi Aprili 16 ambapo atatangaza timu yake ambayo atafanya nayo kazi katika kuibadili klabu hiyo na kuwa klabu bora Tanzania na bara la Afrika.

Alisema kuwa uwepo wa Al Fahim kutaifanya timu hiyo kuwa na uongozi bora wenye kujua uendeshaji wa kisasa katika masuala ya mpira kwa kuzingatia uzoefu wa mfanya biashara huyo mzoefu katika soka na michezo mengine.

“Haikuwa kazi rahisi Al Fahim kukubali kuingia kwenye uongozi wa klabu yetu, ila tunashukuru kwani alituelewa baada ya kukutana naye alipokuja hapa nchini kwa shughuli zake”, alisema Kangezi.

Alisema kuwa lengo lake ni kuona African Lyon inakuwa klabu ya mfano si tu kwa Tanzania, hata kwa nchi za Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla. Kangezi alisema kuwa mipango yao ya awali ni kuimarisha timu ya kwanza ili  iweze kufanya vyema katika mashindano ya ligi kuu na pia kuanzisha msingi mzuri wa timu za watoto.

“Dk Sulaiman ni Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa kampuni ya Al Fahim Group na vile vile alikuwa mkurugenzi wa kituo cha Royal Football Fund (RFF) mbali ya kuwa mchezaji wa mchezo wa chesi, ameahidi kusaidia wachezaji chipukizi ili kuwawezesha kushiriki katika mpira wa kulipwa, tunaamini tutafika,” alisema.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox