Mechi
kati ya Montenegro na Russia ya kutafuta tiketi ya kucheza Euro 2016
iliahirishwa hapo jana mara baada ya matukio kadhaa kutokea uwanjani
Awali
sekundi ya 8 baada ya mpira kuanza kipa wa Russia Igor Akinfeev
alipigwa na moto kichwani na kuzidiwa na hivyo nafasi yake ikachukuliwa
na kipa Yuri Lodygin.
Tukio
hilo lilifanywa na mashabiki wa Montenegro na kusababisa mwamuzi
kusimamisha mchezo huo kwa muda mrefu na baaaye dakika ya 35 ukaendelea .
Hata
hivyo kipindi cha pili mpira ulisimama kwa dakika 18 kufuatia vurugu za
wachezaji wa pande zote 2 na makocha kutokana na mchezaji mwingine wa
Russia kupigwa tena na moto.
Lakini
baadaye dakika ya 66 mwamuzi aliamua kuahirisha mchezo huo baada ya
kipa wa Montenegro Vukasin Poleksic kuokoa penati ya Roman Shirokov
Mpaka pambano hilo lililopigwa nchini Montenegro linaahirishwa timu hizo zilikuwa hazijafungana
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni