Morgan Schneiderlin atakuwa ni wa pili kusajiliwa na klabu ya Manchester United Msimu 2015/2016 na atajiunga na Mashetani wekundu wiki ijayo Jumatano Dirsha la Usajili litakapofunguliwa rasmi. Manchester United wamekamilisha usajili huo kwa kutoa kitita cha £25million kwa Morgan Schneiderlin – na taarifa zaidi kutoka Klabuni humo zinadai kuwa usajili unaendelea na ambao wamewaweka kwenye anga zao ni Kipa Jasper Cillsessen pamoja mchezaji wa Bayern Munich Bastian Schweinsteiger.
Kipa Jasper Cillsessen
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni