STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Ijumaa, 7 Agosti 2015

BARUA YA ANGEL DI MARIA KWA MASHABIKI WA MANCHESTER UNITED


Baada ya kujiunga na PSG kwa dau la paundi milioni 44, winga wa kimataifa wa Argentina, Angel di Maria amewaandikia barua ya wazi mashabiki wa klabu ya Manchester United ambayo ameichezea kwa mwaka mmoja.


Di Maria alisajiliwa na Man United kutokea Real Madrid kwa ada ya paundi milioni 60 na kuvunja rekodi ya usajili ya soka la England.
The Argentina ace completed his move to Ligue 1 champions Paris Saint-Germain on Thursday

BARUA YA WAZI YA ANGEL DI MARIA KWA MASHABIKI WA MANCHESTER UNITED



"Naandika barua hii kuishukuru familia nzima ya Manchester United kwa kuniunga mkono kwa mwaka mmoja niliokuwa sehemu ya klabu.
Manchester United waliponichagua kuwa sehemu ya timu yao, nilijisikia kuheshimiwa kwasababu nilijua klabu hii ina maanisha nini na jinsi gani iliniamini.

Hata hivyo, nafahamu mambo hayakwenda vizuri kama tulivyotarajia, naomba msamaha kwa hilo.

Katika maisha ya mcheza mpira, kuna wakati mwingine mambo usiyotarajia na usiyoyataka yanatokea.

Nawahakikishia kwamba haikuwa kujaribu. Nilijitahidi niwezavyo, lakini mpira sio kama hesabu: Mara zote kuna vitu vingi vinavyoathiri vile unavyofikiria.
Samahani sana kwasababu sikufanya kile nilichotarajia katika klabu hii kubwa na ya ajabu.

Natoa shukurani za pekee kwa bodi ya wakurugenzi na utawala ya Manchester United, vilevile kila kiongozi na wachezaji wenzangu walioniunga mkono.
Pia shukurani za pekee ziwaendee mashabiki ambao mara zote waliniamini na kuonesha heshima na mapenzi makubwa.

Sasa ni wakati wa kujiunga na PSG, lakini Utukufu wa Manchester United utabaki kwenye kumbukumbu zangu daima.
Nawatakia kila la kheri
Angel di Maria".

The 27-year-old attacking midfielder was welcomed to PSG on the club's official Twitter account on Thursday

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox