STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Ijumaa, 7 Agosti 2015

MUSA HASSAN MGOSI APEWA CHEO HIKI NDANI YA KIKOSI CHA SIMBA


Kocha mkuu wa Simba, Muingereza, Dylan Kerr amemteua mshambuliaji mkongwe wa klabu hiyo, Musa Hassan Mgosi kuwa nahodha mpya.

Akizungumza na MPENJA SPORTS mchana huu, kocha msaidizi wa Simba, Seleman Matola amethibitisha uteuzi huo na kusema kwamba waliokuwa manahodha wa klabu hiyo, Hassan Isihaka na Jonas Mkude wanatakiwa kuendelea kujifunza kwa nahodha mpya ambaye ana uzoefu mkubwa.

"Kocha ameangalia uzoefu, nahodha anatakiwa mtu kama Mgosi, anaweza kuongea na wachezaji, anahamasisha timu, ndio maana ameteuliwa".

"Timu inaweza kuwa na manahodha wanne, lakini Isihaka na Mkude wataendelea kujifunza kwa Mgosi, pindi anapoondoka wataweza kurithi nafasi yake". Amefafanua Matola.

Kwa upande wake, Mgosi amefurahia uteuzi huo na kuahidi kuunganisha timu.
"Majukumu yangu ni kuunganisha timu pamoja, kocha ameangalia uzoefu wangu, bila shaka nitaifanya kazi hiyo ipasavyo". Amesema Mgosi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox