STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Ijumaa, 15 Januari 2016

KIM POULSEN AREJEA BONGO KUFUNDISHA SOKA................

 
 
  KOCHA Mdenmark, Kim Poulsen yupo nchini kukamilisha mipango ya Mkataba wa kufundisha timu za vijana za taifa.

Kim, anarejea nchini baada ya mwaka mmoja na ushei tangu aondolewe kufundisha timu ya taifa ya wakubwa, Taifa Stars na nafasi yake kuchukuliwa na Mholanzi, Mart Nooij aliyeondolewa pia Agosti mwaka jana.
 
 
 
 

 
 
 
 
 
 
 
 
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 56, alitua nchini kwa mara ya kwanza Aprili 2011 kufundisha timu za vijana kabla ya Mei 2012 kupandishwa Taifa Stars, kufuatia kuondolewa kwa Mdenmark mwenzake, Jan Borge Poulsen.

Hata hivyo, mapema mwaka 2014 Kim aliondolewa Taifa Stars baada ya kumaliza Mkataba wake na kuajiriwa Mholanzi, Nooij huku Mdenmark huyo akienda Silkeborg IF ya kwao.

Akiwa Taifa Stars, Kim alishinda mechi tano tu kati ya 18, huku akifungwa saba na kutoa sare sita,

Mechi za kukumbukwa alizoshinda Kim ni dhidi ya Gambia 2-1 Kufuzu Kombe la Dunia, dhidi ya Zambia 1-0 kirafiki, dhidi ya Cameroon 1-0 kirafiki na dhidi ya Morocco 3-1 Kufuzu Kombe la Dunia.

Kim aliiongoza timu ya Bara, Kilimanjaro Stars katika mechi 12 za Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge, akishinda tano, sare nne na kufungwa tatu.
 
 
                     
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
                                REKODI YA KIM POULSEN STARS

Jumla ya Mechi; 18
Mechi alizoshinda;          5
Mechi alizofungwa;        7
Mechi alizotoa sare;       6

                     
                   MECHI ZA TAIFA STARS CHINI YA KIM POULSEN;

Mei 26, 2012
Tanzania 0 – 0 Malawi (Kirafiki)
Juni 2, 2012
Ivory Coast 2 – 0 Tanzania (Kufuzu Kombe la Dunia)
Juni 10, 2012
Tanzania 2 – 1 Gambia (Kufuzu Kombe la Dunia)
Juni 17, 2012
Msumbiji 1 – 1 Tanzania (Tanzania ilitolewa kwa penalti kufuzu Mataifa ya Afrika)
Agosti 15, 2012
Botswana 3 – 3 Tanzania (Kirafiki)
Novemba 14, 2012
Tanzania 1-0 Kenya (Kirafiki)
Desemba 22, 2012
Tanzania 1-0 Zambia (Kirafiki)
Januari 11, 2013
Tanzania 1-2 Ethiopia (Kirafiki)
Februari 6, 2013
Tanzania 1-0 Cameroon (Kirafiki)
Machi 24, 2013
Tanzania 3-1 Morocco (Kufuzu Kombe la Dunia)
Juni 2, 2013
Sudan 0 – 0 Tanzania (Mechi ya kirafiki Ethiopia)
Juni 8, 2013 
Morocco 2-1 Tanzania (Kufuzu Kombe la Dunia)
Juni 6, 2013 
Tanzania 2-4 Ivory Coast (Kufuzu Kombe la Dunia)
Julai 13, 2013
Tanzania 0-1 Uganda (Kufuzu CHAN)
Julai 27, 2013
Uganda 3-1 Tanzania (Kufuzu CHAN)
Septemba 7, 2013
Gambia 2-0 Tanzania (Kufuzu Kombe la Dunia)
Tanzania 0-0 Zimbabwe (Kirafiki Dar)
Namibia 1-1 Tanzania (Kirafiki Windhoek)


                       REKODI YA KIM KOMBE LA CECAFA CHALLENGE

Jumla ya mechi alizocheza;   12
Mechi alizoshinda; 5
Mechi alizofungwa; 3
Mechi alizotoa sare; 4

                 MATOKEO YA KILIMANJARO STARS CHINI YA POULSEN;

Novemba 25, 2012
Tanzania  2–0  Sudan (Kundi B)
Novemba 28, 2012
Tanzania  0–1 Burundi (Kundi B)
Desemba 1, 2012
Tanzania 7-0 Somalia (Kundi B)
Desemba 3, 2013
Tanzania 2-0 Rwanda (Robo Fainali)
Desemba 6, 2012
Tanzania 0–3 Uganda (Nusu Fainali)
Desemba 8, 2012
Tanzania  1-1 Zanzibar (Zanzibar ikashinda penalti 6-5) 
Novemba 28, 2013
Tanzania 1-1  Zambia (Kundi B)
Desemba 1, 2013
Tanzania 1-0 Somalia (Kundi B)
Desemba 4, 2013
Tanzania 1-0   Burundi (Kundi B)
Desemba 7, 2013
Tanzania 2-2 Uganda (Robo Fainali, Stars ikashinda kwa penalti 3-2)
Desemba 10, 2013
Tanzania 0-1 Kenya (Nusu Fainali)
Tanzania 1-1 Zambia (Mshindi wa tatu, Zambia wakashinda kwa penalti)

Taifa Stars ya Kim Poulsen ilizifunga Cameroon, Morocco, Zambia na Gambia


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox