STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Ijumaa, 1 Januari 2016

SIMBA YAANZA MWAKA KWA USHINDI, IBRAHIM AJIBU AOKOA JAHAZI


Mabingwa wa kombe la mapinduzi Simba SC wameuanza vyema mwaka 2016 kwa ushindi wa goli moja bila mbele ya Ndanda FC na kupanda mpaka nafasi ya 3 wakiishusha mtibwa sugar hadi nafasi ya 4.

Katika mchezo wa leo uliochezwa katika uwanja wa Nangwanda sijaona uliaribiwa na ubovu wa uwanja na kupelekea kipindi cha kwanza kutumika mipira mirefu zaidi huku wachezaji wakiteleza kutokana na mvua iliyonywesha asubuhi ya leo katika mkoa wa Mtwara. 

Simba SC walipata kona zaidi ya saba katika kipindi cha kwanza lakini wakishindwa kuzitumia, huku Ndanda Fc wakifika langoni mwa Simba SC mara 5.

Kipindi cha pili Simba SC walianza kwa mabadiliko ya kumpumzisha Kiongera na kuingia Ibrahim Ajibu mabadiliko yaliyo wapa utawala wa mchezo simba SC na kuanza kucheza soka la kuonekana japo uwanja ulikuwa hauruhusu.

Katika dakika ya 62 Kocha Kerr alimpumzisha Brian Majegwa na kumuingiza Said Khamisi Ndemla na kuplekea kuongeza kwa kasi ya ushambuliaji ya Simba SC.

Krosi ya Danny Lyanga katika dakika ya 80 na kumkuta Hamisi Kiiza ambapo shuti lake liligonga mwamba na kumuta Ibrahim Ajibu na kuipatia Simba SC goli pekee la ushindi katika mchezo wa leo.

kuingia kwa goli hilo kuliongeza umakini kwa Simba SC na kupelekea mchezo kumalizika kwa simba sc kuibuka na ushindi wa goli 1-0 na kushika nafasi ya 3.
Ligi Kuu inakwenda mapumzikoni kwa mara nyingine hadi katikati ya mwezi, kupisha michuano ya Kombe la Mapinduzi inayoanza keshokutwa visiwani Zanzibar. 
 
Kikosi cha Ndanda FC kilikuwa; Abraham Chove, Bryson Raphael, Ahmed Msumi, Salvatory Ntebe, Jackson Mkwera, Aziz Sibo/Mohammed Ally dk72, Omary Mponda, Hemed Kotta, Kiggi Makassy, William Lucian ‘Gallas’ na Atupele Green, 

 
Simba SC; Vincent Angban, Emery Nimubona, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Abdi Banda, Juuko Murshid, Justice Majabvi, Brian Majwega/Said Ndemla dk65, Mwinyi Kazimoto/Awadh Juma dk89, Paul Kiongera/Ibrahim Hajib dk46, Danny Lyanga na Hamisi Kizza.   


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox