KLABU ya Barcelona
inadaiwa bado inaendelea kuilipa Liverpool kutokana na mauzo ya Luis
Suarez ambapo malipo ya mwisho yanatarajiwa kufanywa Julai mwaka
huu.
Mtandao wa Football Leakes umekuwa ukitoa nyaraka muhimu
zilizohusisha usajili wa wachezaji nyota akiwemo Gareth Bale, Mesut Ozil
na Anthony Martial kwa kipindi cha miezi kadhaa na sasa wamehamia
katika usajili wa Suarez kwenda Barcelona.
Nyota huyo wa kimataifa wa
Uruguay alihamia Camp Nou mwaka 2014 kipindi kifupi baada ya kusababisha
utata mkubwa kwa kumng’ata beki wa Italia Giorgio Chiellini katika
Kombe la Dunia.
Nyaraka zilizovuja zinaonyesha Liverpool walikuwa na nia
ya kuachana na mshambuliaji huyo haraka kutokana na tukio alilofanya
tofauti ya dili zingine nyingi zinazohusiana na masuala hayo ya
usajili.
Taarifa kwenye nyaraka
hizo zimeonyesha kuwa hakukuwa na masharti yeyote yaliyoweka kama ada
ya kununulia au malipo mengine ya ziada kama Barcelona wakishinda taji
la Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Badala yake ilikuwepo ada ya moja kwa moja ya
paundi milioni 64.98 kwa ajili ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 29
ambaye katika kipindi hicho alikuwa amefungiwa miezi minne, na ilitakiwa
kulipwa kwa kidogo kidogo kwa kipindi kwa awamu tano.
Kila awamu
Barcelona walitakiwa kulipa kiasi cha paundi milioni 13, wakianza majira
ya kiangazi alipouzwa na sasa klabu hiyo inatarajia kumaliza awamu yake
ya mwisho Julai 31 mwaka huu.
Kiwango hicho cha ada kilichovuja
kinathibitisha kuwa Suarez ni mchezaji wanne ghali katika historia ya
soka akiachwa kwa karibu na nyota mwenzake wa Barcelona Neymar na nyota
wa Real Madrid Cristiano Ronaldo na Gareth Bale.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni