STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumapili, 27 Machi 2016

BAADA YA CHAD KUJITOA CAF YATOA TAMKO, HUENDA IKATUATHIRI WATANZANIA, YAPIGWA FAINI NA KUFUNGIWA


Timu ya taifa ya Chad imejiondoa kwenye mashindano ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Mataifa ya Afrika, AFCON kwa mwaka 2017 nchini Gabon. 

Chad iliyokuwa imepangwa kundi G lenye timu za Tanzania, Nigeria na Misri imelazimika kujiondoa mashindanoni sababu kubwa ikiwa ni ukosefu wa fedha uliolikumba taifa hilo.

Katika barua yake iliyotumwa kwa Shirikisho la kandanda la Tanzania, Chad imeelezea ‘ukata’ unaowakabili hali iliyopelekea kushindwa kusafiri kutoka nchini kwao kufika Jijini Dar es salaam.

Kiukweli, nchi yetu inapitia kipindi kigumu cha matatizo ya uchumi na kwa upana ushiriki wetu kwenye mashindano mbalimbali umekuwa wa kuishia njiani kwa sababu ya ukosefu wa fedha. Ilieleza taarifa iloyopo kwenye barua hiyo.

Chad inajitoa baada ya kukamilisha mechi tatu za mzunguko wa kwanza, ikifungwa zote 2-0 na Nigeria ugenini, 5-1 na Misri nyumbani na 1-0 na Tanzania nyumbani Jumatano.
  Sasa Kundi G linabaki na timu tatu ambazo ni Tanzania, Nigeria na Misri. Chad hawajaja Tanzania na maana yake mechi ya kesho na Taifa Stars haitakuwepo, lakini bado CAF haijatoa taarifa yoyote juu ya hilo.

Mpaka sasa, Chad inashikilia mkia kwenye kundi lao ikiwa haina alama hata moja huku Misri ikiongoza kundi hilo ikiwa na alama 7 ikifuatiwa kwa ukaribu na Nigeria yenye alama 5 na Tanzania ikiwa na alama 4.

Mchezo wa kwanza uliochezwa Jijini, D,njamena nchini Chad kati ya Tanzania ulimalizika kwa kukubali kichapo cha bao 1-0 huku nahodha mpya wa Tanzania, Mbwana Samatta akikiongoza vizuri kikosi chake kwa kuwa ndiye aliyefunga bao hilo pekee lililoipa ushindi Tanzania.
 
Chad inajitoa baada ya kukamilisha mechi tatu za mzunguko wa kwanza, ikifungwa zote 2-0 na Nigeria ugenini, 5-1 na Misri nyumbani na 1-0 na Tanzania nyumbani Jumatano.

Sasa Kundi G linabaki na timu tatu ambazo ni Tanzania, Nigeria na Misri.
Chad hawajaja Tanzania na maana yake mechi ya kesho na Taifa Stars haitakuwepo, lakini bado CAF haijatoa taarifa yoyote juu ya hilo.


BAADA YA KUJITOA 

Kujitoa kwa Chad katika mechi za kuwania kucheza Afcon huenda likawa jambo jema.

Kwa hali ilivyo, kila timu italazimika kudondosha pointi moja kutoka katika Kundi G iliyopo Stars.

Hivyo, Stars yenye pointi 4, itabaki na pointi moja tu, Nigeria itabaki na pointi mbili huku Misri ikibaki kileleni na pointi 4.

Jambo hilo linapoteza kabisa matumaini ya Taifa Stars huku ikiacha matumaini makubwa kabisa kwa Misri hasa kama itashinda mechi yake dhidi ya Nigeria, keshokutwa.


Kama Misri itashinda, basi itakuwa imefuzu kucheza Afcon kwa asilimia 95.

Tayari Stars ilikuwa imecheza mechi tatu, ilianza kwa kupoteza dhidi ya Misri ugenini, ikatoka sare ya bila mabao na Nigeia jijini Dar es Salaam kabla ya kushinda kwa bao 1-0 mjini ND'jamena dhidi ya wenyeji Chad ambao wamejitoa kwa madai hawana nauli.
 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox