STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 17 Machi 2016

LIGI KUU BARA...HUYU NDIYE BINGWA MSIMU HUU!!!




MEI 7, mwaka huu msimu wa 2015/16 unatarajiwa kufikia tamati kwa timu zote 16 kushuka viwanjani katika mikoa tofauti, hiyo itakuwa ni baada ya mikikimikiki ya takribani miezi nane tangu msimu ulipoanza Septemba 12, mwaka jana.




 Ligi hiyo ambayo kwa sasa inaongozwa na Simba, inazishirikisha timu 16, na baada ya msimu kumalizika timu tatu zitashuka daraja huku tatu kutoka Ligi Daraja la Kwanza zikija kuziba nafasi zao kwa ajili ya msimu ujao. 

Takribani mechi saba mpaka kumi zimebaki kwa timu zote kukamilisha msimu, lakini mpaka sasa hakuna timu iliyojihakikishia ubingwa wala zile zitakazoshuka hazijajulikana rasmi licha ya kuwepo zinazotajwa kuwa kwenye hatari ya kushuka kwa jinsi mwenendo wao ulivyo. 


Vita ya kuwania ubingwa mpaka sasa ipo kwa timu tatu, Simba, Yanga na Azam ambazo ndizo zimepishana pointi chache tofauti na ile inayofuata baada ya hizo.

 Simba ipo kileleni na pointi zao 54, hiyo ni baada ya kucheza mbili zaidi ya Azam na Yanga. Katika michuano mbalimbali, kila timu huwa inaringia uwanja wake wa nyumbani inaoutumia kwa mechi zake, katika mechi saba zilizobaki za Simba, nne watacheza nyumbani na tatu pekee watalazimika kwenda ugenini. 

Tunapozungumzia viwanja vya nyumbani kwa timu hizi tatu, tunamaanisha Uwanja wa Taifa unaotumiwa na Yanga na Simba na Uwanja wa Azam Complex ambao Azam FC huutumia kwa mechi zao za nyumbani, lakini inapocheza na Yanga au Simba, wanalazimika kwenda Taifa na kuonekana kama wapo ugenini japo ratiba inaonyesha wao ndiyo wapo nyumbani.

 Yanga nayo mechi zao tisa zilizobaki, nne pekee watacheza nyumbani na tano ugenini huku Azam mechi zao tisa, nne watacheza nyumbani na tano ugenini.

 Katika hesabu zilizofanywa na mchambuzi wa makala hii na kama zikienda sawia, bila shaka bingwa wa msimu huu tayari kashajulikana.

 Simba Ilianza vizuri msimu huu kwa kushinda mechi mbili mfululizo ugenini kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga ambapo awali palionekana kuwa kikwazo kwao, lakini ikiwa chini ya Muingereza aliyetimuliwa kikosini hapo, Dylan Kerr wakaweza kuondoka na pointi zote sita kwenye mechi zao mbili walizocheza uwanjani hapo, dhidi ya JKT Mgambo na African Sports.

 Hakuna asiyefahamu kama ukienda ugenini lazima upate shida kuondoka na pointi, lakini ukiangalia rekodi ya Simba msimu huu, imeshinda ugenini mechi sita kati ya tisa, sare moja na imefungwa mbili. 

Kumbuka imebakiwa na mechi tatu ugenini, dhidi ya Coastal Union, Majimaji na Mtibwa.

 Kwa jinsi mechi hizo zilivyo, wanaweza wasipate kikwazo sana watakapocheza na Majimaji, lakini hizo zingine kupata pointi ni nusu kwa nusu. 

Ukiachana na mechi za nje ya Dar, Simba imecheza mechi 14 ndani ya Uwanja wa Taifa, imeshinda 11, sare moja dhidi ya Azam na imepoteza mbili ambazo zote ni dhidi ya Yanga huku bado ikiwa haijacheza tena na Azam uwanjani hapo.

 Yanga Inashika nafasi ya pili kwa sasa ikiwa na pointi 50, imebakiwa na michezo tisa kabla ya kuhitimishwa kwa ligi. 

Ikifanikiwa kushinda mechi zake mbili ili kuwa sawa na Simba kimichezo itafikisha pointi 56, inaweza kukaa kileleni kutokana na kuwa na wastani mzuri wa mabao. 

Katika mechi zake 21 ilizocheza mpaka sasa, 14 imechezea nyumbani na saba ugenini.

 Katika hizo, nyumbani imeshinda 12, sare mbili ambazo zote ni dhidi ya Azam. Ikiwa ugenini, imeshinda tatu, sare tatu na imepoteza moja.

 Katika mechi zilizobaki itaenda ugenini mara tano. Kikwazo kwao kinaweza kuwa kwa Ndanda na Mbeya City kutokana na rekodi yao huko nyuma, lakini kwa timu zingine za Majimaji, Stand United na Toto African inaweza isikumbane na changamoto kubwa sana kwa jinsi rekodi yao inavyosema inapocheza huko.

 Nyumbani imebakisha mechi nne, ukiziangalia kwa jicho la mbali hakuna itakayoweza kuinyima Yanga pointi ukizingatia kwamba mpaka sasa haijapoteza nyumbani. Mtibwa, Kagera, Mgambo na Mwadui ndizo itacheza nazo nyumbani.

 Azam Mechi zake tisa zimebaki kumaliza msimu. Inashika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 50, endapo itashinda mechi zake mbili ili kuwa sawa na Simba kimichezo, itafikisha pointi 56 sawa na Yanga kama nayo itachanga vizuri karata zao kwa viporo vyao, hapo watakuwa wanaiacha Simba kwa pointi mbili. 

Azam italazimika kusafiri kutoka nyumbani kwao kwenda ugenini mara tano kama ilivyo kwa Yanga. Katika mechi 21, Azam imecheza tisa nyumbani na kushinda nane, sare moja huku ikiwa haijapoteza hata mchezo mmoja.

 Kwa michezo ya ugenini, imecheza 12, imeshinda saba, sare nne na imepoteza mmoja.

 Katika mechi za nyumbani zilizobaki haiwezi kupata shida sana kwenye kusaka ushindi, lakini wanapaswa kuwa makini na Mgambo. 

Zingine ambazo ni Ndanda, Stand, JKT Ruvu na Majimaji uwezo wa kushinda ni asilimia 70. Ugenini, itakumbana na Simba na Mtibwa, hizi ndizo mechi ngumu kwao, lakini zilizobaki dhidi ya Toto African, African Sports na Kagera Sugar si kikwazo sana kwao.



Hitimisho Kutokana na takwimu hizo na jinsi mechi za ugenini zilivyokuwa ngumu, tumebaini kwamba zote zina mechi mbili ngumu huko, ni jukumu lao kuzichanga vyema karata zao ili kuepuka majanga ya kudondosha pointi, kama moja ikiteleza basi inaweza kuwa ndiyo basi tena katika mbio za kuwania ubingwa, lakini kama zote zitakaza na kupata matokeo mazuri, bila shaka Yanga ndiyo inayo nafasi kubwa ya kuwa bingwa, Azam ya pili na Simba ya tatu.

 Hakuna aijuaye kesho, tusubiri tuone mwisho wake. 

 
              
                 Mechi zilizobaki kwa Yanga;

 Yanga Vs Mtibwa Taifa 
Toto Vs Yanga Kirumba 
Yanga Vs Mwadui Taifa
 Yanga Vs Kagera Taifa 
Stand Vs Yanga Kambarage
Yanga Vs Mgambo Taifa
 Mbeya City Vs Yanga Sokoine 
Ndanda Vs Yanga Nangwanda
Majimaji Vs Yanga Majimaji 

 
          
                  Mechi zilizobaki kwa Azam;

 Mtibwa Vs Azam Manungu 
Azam Vs Ndanda Azam Complex 
Azam Vs Stand Azam Complex
 Azam Vs JKT Ruvu Azam Complex
 Toto Vs Azam Kirumba 
Azam Vs Majimaji Azam Complex
 Simba Vs Azam Taifa
 Kagera Vs Azam Mwinyi 
African Sports Vs Azam Mkwakwani
 Azam Vs Mgambo Azam Complex 





             Mechi zilizobaki kwa Simba;

 Coastal Vs Simba Mkwakwani 
Majimaji Vs Simba Majimaji 
Simba Vs Toto Taifa 
Simba Vs Azam Taifa 
Simba Vs Mwadui Taifa 
Mtibwa Vs Simba Jamhuri 
Simba Vs JKT Ruvu Taifa


                                                           
                                                      www.mdosejr@gmail.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox