TAIFA la China
limezindua mikakati yake ya kuja kuwa taifa lenye nguvu kisoka ifikapo
mwaka 2050, kwa mipango ya kupata vijana wadogo na wakubwa zaidi ya
milioni 50 wachezaji soka ifikapo mwaka 2020.
Malengo mengine
yanajumuisha kuwa na walau vituo vya soka 20,000 kwa ajili ya mazoezi na
viwanja 70,000 ifikapo mwaka 2020.
Wakati China ikifanya vyema katika
michuano ya Olimpiki na Paralimpiki, taifa hilo limefanikiwa kufuzu mara
moja pekee katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2002.
Rais wa China
Xi Jinping ameonyesha kuwa na shauku kubwa katika soka ambapo mara
kadhaa amekuwa akikaririwa akidai kuwa anataka taifa hilo kutwaa Kombe
la Dunia katika kipindi cha miaka 15 ijayo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni