Goalkeeper: Keylor Navas (Real Madrid)
Right back: Dani Alves (Barcelona)
Right centre back: Gerard Pique (Barcelona)
Left centre back: Sergio Ramos (Real Madrid)
Left back: Marcelo (Real Madrid)
Right midfield: Ivan Rakitic (Barcelona)
Holding midfield: Sergio Busquets (Barcelona)
Left midfield: Andres Iniesta (Barcelona)
Right attack: Lionel Messi (Barcelona)
Centre forward: Luis Suarez (Barcelona)
Left attack: Neymar
NAHIVI NDIVYO KIKOSI KINAVYOJIPANGA
Barcelona forward Neymar (left) beats Cristiano Ronaldo and Gareth Bale to a place in our combined XI
El Clasico ya Jumamosi itakayowakutanisha wapinzani
wakubwa Barcelona na Real Madrid katika uwanja wa Camp Nou itampa
Zinedine Zidane fursa ya kuonyesha uwezo wake
Akiwa anelekea kuiogoza timu yake kucheza Clasico kwa mara ya kwanza kama kocha, Zidane mwenye miaka 43 anahitaji kuonyesha uwezo wake kama kiongozi.
Kwa upande mwingine, bosi wa timu ya nyumbani Luis Enrique amefanikiwa kuzishinda changamoto nyingi anazokumbana nazo Zidane sasa.
Licha ya mafanikio yanayoonekana, aliufurahia msimu uliopita, miezi michache ya kwanza ya Enrique ilikuwa rahisi sana, hakupata ugumu wowote.
Mara kadhaa alibadili watendaji wa timu na mikakati, na alikumbwa na mlolongo wa matokeo mabovu ikiwa ni pamoja na kupoteza mechi ya Clasico kwa kipigo cha 3-1 hivyo kuibua tetesi kuwa kibarua chake kilikuwa hatiani kabla ya timu yake kubadili mwelekeo na kufanya maajabu msimu wote.
Wiki za awali za uongozi wa Enrique, Barca kilionekana kama kikosi cha wachezaji ambao walikuwa wakitegemea uwezo wao binafsi kuliko kushiriki mipango ya mchezo kwa pamoja – Naam, kama ilivyo kwa Real Madrid ya sasa.
Zidane na Enrique walikutana mara kadhaa dimbani katika mechi za Clasico, moja ya mechi ni ile ya 2003 iliyopigwa Bernabeu ambayo Enrique alikiri kutoikumbuka vizuri.
Lakini sasa, Zidane anajaribu kubadili kikosi chake kilichosheheni vipaji na kurahisisha kazi kwa kuijenga timu icheze kwa ushirikiano kuliko kundi la wachezaji wasiokuwa na maelewano.
Ni lazima Zidane atumia vizuri uwezo wa Ronaldo
Kwa namna ambayo Enrique alipata changamoto kubwa alipowasili Barcelona kupanga mfumo wa uchezaji ambao ulimwezesha kupata mafanikio zaidi kupitia Lionel Messi bila ya kuvuruga ufanisi wa timu, ndivyo Zidane anavyofanya kujenga mfumo thabiti na kukitumia vizuri zaidi kipaji cha Cristiano Ronaldo.Umekuwa msimu wa tofauti kwa Mreno huyo mwenye miaka 31. Kwa upande mwingine ni kinara wa magoli wa La Liga akiwa na mabao 28 katika mechi 30, kwa hiyo ni mpambanaji.
Lakini mengi ya mabao yake yamepatikana katika mechi walizoshinda kwa kishindo tu – manne dhidi ya Celta Vigo (ushindi wa 7-1); matatu dhidi ya Espanyol nyumbani (6-0); matano dhidi ya wapinzani hao hao ugenini (6-0) – na ameshindwa kufanya maajabu timu yake ilipokutana na timu ngumu.
Ronaldo alipondwa baada ya kushindwa kung’ara Madrid ilipochezea kichapo kutoka kwa Atletico, na mara nyingi ameshindwa kutamba katika mechi za ugenini nje ya Bernabeu akifunga mara mbili tu kati ya mechi tisa za ligi.
Lakini Zinedine ametumia kila fursa kutumia uwezo na umuhimu wa nyota huyo wa zamani wa Manchester United.
Katika wiki yake ya kwanza kazini, Zidane alithubutu kuzima tetesi kuhusu mustakabali wa Ronaldo: “Cristiano si mchezaji wa kuhama. Ni roho ya timu. Nikiwa hapa hataondoka.”
Uhusiano wao mzuri ulidhihirika Ronaldo alipokuwa akishangilia goli lake la Ligi ya Mabingwa Roma mwezi Februari alipokimbia kumkumbatia kocha wake.
Tukio hilo lilionesha faida tofauti aliyo nayo Zidane dhidi ya mtangulizi wake Benitez – na, kwa hali kadhalika Enrique siku zake za awali katika Barcelona.
Utatu wa Real Madrid ‘BBC’ Unahitaji kufanya kazi kwa ushirikiano
Ronaldo si mchezaji pekee muhimu kwa Real Madrid wanapoelekea Clasico ya wikiendi, wengi wanatarajia kuona kitu kutoka kwa utatu wao wa BBC – Gareth Bale na Karimu Benzema (na C kwenye BBC ikisimama kwa Cristiano).Wote wapo kwenye kiwango safi baada ya majeraha, baada ya Benzema kutumia dakika sita tu kufunga goli katika ushindi wa 4-0 dhidi ya Sevilla kabla ya mapumziko ya kimataifa.
Katika mechi hiyo Bale alifunga bao baada ya kugonga besela, na alitoa pasi ya bao, pia anatarajiwa kufanya makubwa katika mechi ya Jumamosi.
Mwisho wa yote, mafanikio ya BBC yanategemea uwezo wa Zidane kuwaunganisha kuwa kitu kimoja kuliko kuwaachia uhuru wa kila mmoja kufanya kila atakacho ambayo ni tabia ya Ronaldo hasa – na kuwapa wakati mgumu mabeki wa Barca.
Kama vile Messi alivyofaidika na ushirikiano wa Luis Suarez na Neymar, jukumu la Ronaldo kuipa mafanikio Real litakuwa rahisi kama atakubali usawa baina yake na Bale na Benzema kama marafiki na wasaidizi badala ya tishio la hadhi yake, kama inavyoonekana mara zote.
Ni kazi ya Zidane kuunda utatu madhubuti kama kocha mahiri na mwenye ushawishi.
Jinsi Madrid watakavyojipanga katika uwanja wa Camp Nou
Tangu kupoteza dhidi ya Atletico, Zidane amekuja na mkakati tofauti wa kutumia mfumo wa 4-3-3, Isco akiachwa mara nyingi kwa ajili ya mchezo wa kujihami akimtumia Casemiro pembeni mwa Luka Modric na Toni Kroos kama kiungo cha kati.
Ulinzi madhubuti kwa beki nne umekuwa tatizo tangu Xabi Alonso alipoondoka kujiunga na Bayern Munich, na Casemiro, Kroos, Asier Illarramendi, Sami Khedira, Lucas Silva na hata Sergio Ramos wote kushindwa kutimiliza jukumu hilo.
Lakini Casemiro, ambaye msimu uliopita alikuwa Porto kabla ya kurudi Bernabeu amekuwa akifanya kazi nzuri tangu alipaonza kutumiwa na Zidane, huenda akawa jawabu la tatizo.
Mfumo wa 4-3-3, ambao unatumiwa na Barca, ambapo Ivan Rakitic, Sergio Busquts na Andres Iniesta wamekuwa na maelewano mazuri wakiwasaidia mabeki wao wote wane na utatu wao wa mashambulizi MSN.
Hata kama Modric, Casemiro na Kroos watakuwa na jukumu sawa mafanikio ya Real Madrid yataonekana, lakini ni wazi Zidane atautumia mfumo huu mechi hii ya wikiendi.
Barcelona: Bravo; Alves, Pique, Mascherano, Alba; Rakitic, Busquets, Iniesta; Messi, Suarez, Neymar
Real Madrid: Navas; Danilo, Pepe, Ramos, Marcelo; Kroos, Casemiro, Modric; Bale, Benzema, Ronaldo
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni