YANGA
SC itamenyana na Coastal Union katika Nusu Fainali ya michuano ya
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Kombe la Azam Sports
Federations Cup 2016.
Mchezo
huo utafanyika Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga Aprili 24, mwaka huu,
siku ambayo Azam FC itamenyana na Mwadui FC Uwanja wa Mwadui Complex,
Tanga Aprili 24, mwaka huu pia.
Hiyo
inafuatia droo iliyopangwa jana studio za Azam TV, wadhamini wa michuano
hiyo, Tabata, Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Katibu wa TFF, Selestine
Mwesigwa.
Mshambuliaji
wa zamani wa timu ya taifa ya wanawake, Twiga Stars, Esther Chabruma
ndiye aliyechagua timu za kumenyana katika Nusu Fainali katika droo
hiyo, akisimamiwa na Ofisa Habari wa TFF, Baraka Kizuguto.
Coastal
Union iliingia Nusu Fainali baada ya kuitoa Simba SC kwa kuifunga mabao
2-1, wakati Azam FC iliitoa Prisons kwa kuifunga 3-1, Mwadui FC iliitoa
Geita Gold kwa kufunga 3-0 na Yanga SC iliwafunga Ndanda FC 2-1.
Bingwa
wa Kombe la ASFC, michuano iliyoanza na timu 64 Novemba mwaka jana,
ataiwakilisha Tanzania kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika
mwakani.
Katika
hatua ya awali, kila timu ilipatiwa fedha za usafiri Sh Milioni 3, na
vifaa vya mashindano kutoka kwa wadhamini, Azam TV ikiwa ni sehemu ya
udhamini wa Bilioni 3.3.
Bingwa wa Kombe la ASFC atajinyakuliwa kitita cha Sh. Milioni 50,
Fainali inatarajiwa kuchezwa wiki moja baada ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika.
Mara
ya mwisho michuano hiyo ilifanyika mwaka 2002 na JKT Ruvu ikaifunga
Baker Rangers ya Magomeni katika fainali, wakati ikijulikana kama Kombe
la FAT (Chama cha Soka Tanzania).
ORODHA YA MABINGWA KOMBE LA SHIRIKISHO
1967 Yanga SC
1974 Yanga SC
1985 Maji Maji
1995 Simba SC
1996 Sigara
1997 Tanzania Stars
1998 Tanzania Stars
1999 Yanga SC
2000 Mtibwa Sugar
2001 Yanga SC
2002 JKT Ruvu
Chanzo: Bin Zubeir
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumanne, 12 Aprili 2016
Home
/
Unlabelled
/
HII HAPA RATIBA YA NUSU FAINALI KOMBE LA SHIRIKISHO, YANGA KUVAANA NA "WAARABU WA TANGA"
HII HAPA RATIBA YA NUSU FAINALI KOMBE LA SHIRIKISHO, YANGA KUVAANA NA "WAARABU WA TANGA"
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni