Goli safi la Haruna Niyonzima limeipa pointi tatu muhimu mabingwa wa
ligi kuu ya vodacom Yanga SC mbele ya vijana wa Jamhuri Kihwelo Julio
Mwadui FC mchezo uliocezwa katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.
Katika mchezo huo wa leo uliotawaliwa kila aina ya ufundi, Yanga SC
waliandika goli lao la kwanza katika dakika ya 2 ya mchezo kupitia kwa
Saimon Msuva.
Kuingia kwa goli hilo kuliwafanywa Mwadui kucheza kwa tahadhari kubwa,
na kujaribu kupandisha mashambulizi kadha langoni mwa yanga sc, huku
yanga wakiendeleza kasi yao.
Katika dakika ya 13 Kelvin Sabato aliisawazisha Mwadui FC na kupeleka mchezo kwenda mapumziko wakiwa sare ya goli 1-1.
Kipnid cha pili kilianza kwa kasi, huku yanga wakimuingiza beki Vicent
Bosue kuchukuwa nafasi ya Pato Ngonyani, kitendo kilichoimarisha safu
yao ya ulinzi.
Katika dakika 67 beki wa Mwadui FC Sabo alizawadiwa kadi nyekundu na kupelekea Mwadui FC kumaliza mchezo wakiwa pungufu.
Yanga SC walitumia upungufu huo na kupeleka mashambulizi mfululizo
langoni mwa Mwamdui FC, lakini uimara wa Shaban Kado uliwapeleka yanga
sc kungoja mpaka katika dakika ya 86.
Alikuwa Haruna Niyonzima akimalizia klwa ustadi mpira wa urejesho toka
kwa Donald Ngoma aliyeunga krosi ya Oscar Joshua na kuiandikia Yanga
goli la pili na kupeleka mchezo kumalizka kwa yanga kuibuka na ushindi
wa goli 2-1.
Kwa matokeo hayo ya leo Yanga SC wanafikisha pointi 56 baada ya kucheza
michezo 23 wakiwa nyuma kwa mchezo mmoja dhidi ya vinara Simba SC
wanoangoza ligi kwa tofauti ya pointi 1.
Kikosi
cha Yanga kilikuwa; Deogratius Munishi ‘Dida’, Juma Abdul, Oscar
Joshua, Pato Ngonyani/Vincent Bossou dk46, Nadir Haroub ‘Cannavaro’,
Thabani Kamusoko, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Donald Ngoma, Amissi
Tambwe/Malimi Busungu dk79 na Issoufour Boubacar/Godfrey Mwashiuya dk46.
Mwadui
FC: Shaaban Kado, Malika Ndeule, David Luhende, Iddy Mobby, Joram
Mgeveke/Abdallah Mfuko dk30, Anthony Mataogolo, Jabir Aziz, Razack
Khalifan, Kevin Sabati, Juma Mnyate na Hassan Kabunda/Nizar Khalfan
dk57.
Mchezo mwingine wa Ligi Kuu leo, Azam FC imeshinda 1-0 dhidi ya Mtibwa Sugar Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro.
Shukrani
kwake, Nahodha John Raphael Bocco aliyefunga bao hilo pekee dakika ya
62 kwa penalti baada ya mshambuliaji Kipre Herman Tchetche kuchezewa
rafu kwenye boksi.
AzamFC sasa inafikisha pointi 55 baada ya kucheza mechi 24, ikiendelea kukaa nafasi ya tatu nyuma ya Yanga na Simba.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumatano, 13 Aprili 2016
Home
/
Unlabelled
/
NIYONZIMA AKIWEKA KWENYE "FRIJI" KIPORO CHA YANGA, AZAM WAITAMBIA MTIBWA MANUNGU
NIYONZIMA AKIWEKA KWENYE "FRIJI" KIPORO CHA YANGA, AZAM WAITAMBIA MTIBWA MANUNGU
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni