STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumanne, 5 Aprili 2016

MAJANGA KWA CHELSEA,CONTE ANAKASHFA NZITO KUFUNGIWA JELA LA SOKA......

 Newly-appointed Chelsea manager Antonio Conte is embroiled in Italy's match-fixing scandal

Kiongozi wa mashtaka nchini Italia amependekeza kocha mpya wa Chelsea Antonio Conte kuhukumiwa kifungo cha miezi 6 kwa mchango wake katika kupanga mechi mwaka wa 2011.

Wakili wa Conte amesisitiza kuwa mteja wake hakufanya kosa lolote.

Kocha huyo mpya wa Chelsea anakabiliwa na tuhuma za ''udanganyifu katika michezo'' katika mji wa Cremona Italia.

Kesi hiyo inahusiana na madai kuwa klabu ya ligi ya daraja la pili Serie B.;Siena aliyokuwa akiifunza mnamo mwaka wa 2011 ilihusishwa na kashfa ya upangaji mechi.

 Conte has always maintained his innocence and has described the process as 'spine-chilling'

Konte mwenye umri wa miaka 46 pia aliwahi kuifunza Juventus.
Aliwashangaza wengi alipoteuliwa meneja mkuu Stamford bridge baada ya kuiongoza Italia katika mashindano ya Euro.

Tayari kocha huyo ametumikia marufuku ya shirikisho la soka la Italia kuhusiana na tukio hilo la mwaka wa 2011.

Kiongozi wa mashtaka Roberto di Martino, ametaja mechi kati ya klabu yake na timu ya Albino Leffe, ambayo anadai Conte alifahamu fika jaribio la kupanga matokeo yake.

Amependekeza Conte ahukumiwe kifungo cha miezi 6 na kutozwa fain ya euro 8,000.

Wakili wa Conte , Leonardo Cammarata, anatarajiwa kumtetea mteja wake Aprili 11.

Mahakama itatoa uamuzi wake mwezi Mei.

Msemaji wa waajiri wapya wa Conte Chelsea alikataa kuzungumzia swala hilo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox