SHIRIKISHO
la soka Tanzania (TFF) limekubali kuisogeza mbele mechi ya Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania Bara kati ya mabingwa watetezi, Yanga dhidi ya Mtibwa
Sugar iliokuwa ichezwe Jumatano (Aprili 6, 2016) na badala yake itapigwa
Aprili 16 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Hiyo
inafuatia malalamiko ya Yanga kupangiwa mechi tatu ndani ya wiki moja
kabla ya kumenyana na Al Ahly ya Misri Jumamosi ijayo katika Ligi ya
Mabingwa Afrika.
Maana
yake, Yanga SC watashuka dimbani leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam
kumenyana na Kagera Sugar ya Bukoba katika mfululizo wa Ligi Kuu na
baada ya hapo watakwenda kambini kujiandaa na mchezo dhidi ya Al Ahly
mwishoni mwa wiki.
Akizungumza
na chombo kimoja cha habari leo, Mkuu wa Idara ya Habari na
Mawasiliano ya Yanga, Jerry Murro amesema kwamba mechi hiyo imeondolewa
na badala yake itachezwa Aprili 16, kama ilivyopangiwa na Shirikisho
hilo.
Alisema
kwa matokeo hayo, kikosi hicho baada ya mchezo wa dhidi ya Kagera
Sugar, wataendelea kujifua kujiandaa na mechi dhidi ya Al Ahly
iliyopangwa kufanyika Aprili 9 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kwa
upande wake, Msemaji wa Azam FC, Jaffar Iddi amesema wao wamekataa
kuahirishiwa mchezo wao na Ndanda FC na watashuka dimbani Aprili 6
kumalizia kiporo hicho.
CHANZO;BIN ZUBEIRY
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni