STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumamosi, 18 Juni 2016

MOURINHO NA CONTE WATULIZWA , REAL MADRID WAWEKEWA KIGINGI , ARSENAL NA LEICESTER MH!

 



WAKALA wa nyota wa​ Slovakia  Marek Hamsik amekaririwa akisema kuwa mchezaji huyo ataendelea kusalia Napoli licha ya tetesi zinazoendelea kuwa atajiunga na  Chelsea au Manchester United.




Timu zote zilionesha nia ya kumtaka mchezaji huyo mwenye miaka 28 tangu miezi kadhaa iliyopita huku akiwa katika kiwango bora kwenye michuano ya  Euro 2016. Pamoja na hayo wakala wake Juraj Venglos amekanusha haraka taarifa za mchezaji huyo kujiunga na miamba hiyo ya Uingereza.

Venglos ameiambia ​Radio Crc: "Hamsik tayari yupo kwenye klabu kubwa haoni sababu ya kuondoka.

"Siku chache zijazo nitakutana na Rais  Aurelio De Laurentiis na Mkurugenzi wa michezo  Cristiano Giuntoli, lakini siwezi kuzungumzia mustakabali wa nyota huyo ila hawezi kwenda popote."

Wakati huo huo Hamsik mwenyewe akizungumza na ​Sky Italia, alisema ataongeza mkataba wa kuendelea kubaki na hafikirii kwenda mahali popote.

“Naipenda hii jezi, siku zote nimekuwa nikisema hivyo, bado nina miaka mitano zaidi ya kuendelea kubaki hapa, nina furaha na nitaebdelea kuwepo,” alisema Hamsik.

Hamsik alionyesha kiwango kizuri katika ushindi wa magoli 2-1 wa nchi yake dhidi ya Urusi na Jumatatu atakiongoza kikosi hicho kumenyana na Uingereza katika muendelezo wa michuano ya Euro.


                                        TETESI YA PILI;

JUVENTUS inahitaji dau la kuvunja rekodi ya dunia la pauni 160 milioni toka  Real Madrid ili kumuachia kiungo wake  Paul Pogba katika dirisha hili la usajili.

Kocha wa Madrid  Zinedine Zidane na Rais Florentino Perez wamemfanya kiungo huyo kuwa mchezaji wao namba moja msimu huu sambamba na mchezaji mwenzake wa timu ya taifa ya ufaransa Dimitri Payet.

Los Blancos wanatarajia kumuuza  James Rodriguez ili kupata fedha ya kumchukua Pogba, lakini bei hiyo inaweza kutibua dili hilo huku kiungo huyo pia akiwindwa na Manchester United, Manchester City, Chelsea na Paris Saint Germain.

Gazeti la  Marca la nchini Hispania limeripoti kuwa  Madrid haitokuwa tayari kutoa kitita hicho kwa kiungo huyo mwenye umri wa miaka 23 huku wakala wake Mino Raiola akisema dili hilo litakamilika.

Ripoti zinasema kuwa Juve wanajua Real hawana longo longo katika matumizi ya pesa hasa wanapo muhitaji mchezaji kama walivyowauzia Zidane mwaka 2011 kwa kuvunja rekodi ya dunia ya wakati ule lakini katika hili miamba hiyo ya Hispania inaweza ikachemka.

Zidane ni shabiki mkubwa wa kiungo huyo kitu kinachoipa Real nafasi ya kupata saini yake huku wote wakitokea taifa la Ufaransa.

Pogba kwa sasa yupo na kikosi cha Ufaransa kinacho shiriki michuano ya Euro na tayari ameshaisaidia kupata ushindi wa michezo yake yote miwili ya awali.



                               TETESI YA TATU;

MAKAMU Mwenyekiti wa klabu ya Leicester City, Aiyawatt Srivaddhanaprabha​ anaamini mshambuliaji wao anayewindwa na  Arsenal Jamie Vardy ataendelea kusalia  Kings Power msimu ujao baada ya kuipiga chini ofa ya Washika bunduki hao.

Arsenal walipeleka ofa ya pauni 20 milioni ambayo walikuwa na matumaini ya kukamilisha dili hilo kabla ya kuanza kwa michuano ya Euro 2016. Vardy alichelewa kutoa maamuzi hadi itakapomalizika michuano na sasa klabu yake imempandishia mshahara hadi pauni 100,000 kwa wiki sawa na ambao angelipwa Arsenal.

Akizungumza na gazeti la  Mail, Makamu huyo alisema hatma ya mshambuliaji huyo itajulikana muda mfupi ujao na ana uhakika wa kumbakiza mpachika magoli huyo aliyetisha msimu uliopita.

"Mtapata habari muda si mrefu, lakini nina imani atabaki.
Tunataka kujenga kikosi bora msimu ujao kitakacho washangaza wengi kuanzia kwenye ligi na klabu bingwa.

"Michuano ya klabu bingwa tumepania kufanya vizuri japokuwa wengi wanatuona kama ni wachanga, na hatutishiki na uchanga wetu," alimaIizia Aiyawatt.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox