STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatano, 17 Agosti 2016

AZAM WAIFANYA KITU MBAYA YANGA, WABEBA NGAO, KESSI, NIYONZIMA "WACHOMESHA"

Mabingwa wa Afrika mashariki na kati Azam FC wamefanikiwa kutwa ngao ya jamii kwa mara ya kwanza baada ya kuwafunga yanga sc kwa mikwaju ya penati 4-1, baada ya dakika 90 kumalizika kwa sare ya ya goli 2-2.

 
Katika mchezo huo ulishuhudia Azam FC wakifanya shambulizi lao la kwanza katika lango la yanga katika dakika ya 30 ikiwa ni baada ya yanga kuwa mbele kwa goli 2-0.

Katika dakika zote 30 za mwanzo Yanga SC walitawala vilivyo mchezo na kufanikwa kupata magoli mawili yaliyofungwa na Donald Ngoma katika dakika ya 20 kwa mkwaju wa penati na 22 akimalizia pasi ya Hassan Kessi.

Katika kipindi cha pili Azam FC walianza kwa mabadiliko ya kumtoa Ramadhani Singano na kumuingiza Mudathir Yahya kitendo kilichorejesha mchezo kuwa sawa kwa pande zote mbili huku wakishambuliana kwa zamu.

Alikuwa Shomari Kapombe alieandikia Azam Fc goli la kwanza katika dakika ya 75 kabla ya John Bocco kuifungia Azam FC goli la kusawaizsha kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 90 na kupeleka dakika 90 kumalzika kwa sare ya goli 2-2.

Katika mikwaju ya penati Azam FC walipata penati zote nne wakati yanga wakipata penati moja iliyopigwa na Deo Munish Dida huku Haruna Niyonzima na Hassan Kessi wakikosa penati.

Penati za Azam Fc zilifungwa na Himid Mao, John Bocco, Michael Bolue na Shomari Kapombe wakipata penati za Azam FC

Azam FC inatwaa Ngao ya Jamii kwa mara kwanza baada ya kuwania bila mafanikio mara nne kuanzia mwaka 2012 ikifungwa na Simba SC 3-2, kabla ya kuanza kufungwa mfululizo na Yanga 1-0 mwaka 2013, mwaka 2014 mabao 3-0 na mwaka jana kwa penalti 8-7 kufuatia sare ya 0-0.
 
Kikosi cha Yanga SC kilikuwa; Deogratius Munishi ‘Dida’, Hassan Kessy, Mwinyi Hajji Mngwali, Mbuyu Twite, Vincent Bossou, Said Juma ‘Makapu’, Haruna Niyonzima, Juma Mahadhi/Malimi Busungu dk81, Thabani Kamusoko, Amissi Tambwe/Simon Msuva dk67 dk na Donald Ngoma.

 
Azam FC; Aishi Manula, Isamil Adam, Bruce Kangwa, David Mwantika, Himid Mao, Jean Baptiste Mugiraneza, Shomary Kapombe, Salum Abubakar ‘Sure Boy’/Kipre Balou dk90, John Bocco, Shaaban Chilunda/Mudathir Yahya dk46 na Ramadhani Singano ‘Messi’/Francesco Zekumbariwa dk46. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox