Kamati ya Utendaji ina mamlaka ya kuitisha mkutano huo kwa mujibu wa Katiba ya Simba Ibara ya 22 kifungu cha kwanza ambapo nyaraka za mkutano huo zitatolewa kwa wanachama wao kupitia matawi yote ya Simba kwa muongozo wa Ibara ya 22 kifungu cha nne cha Katiba yao.
Hata hivyo Kiganja, amesisitiza kuwa, Katiba ya Simba iliyopo na inayotambuliwa kwa msajili ni ile ya 2010 ambayo ina mapungufu mengi hivyo wanapaswa kuwa makini na ili mchakato huo ukamilike na kupitishwa ni lazima msajili wa vyama vya michezo aikubali na kugonga mhuri na si vinginevyo.
"Wafanye mkutano wao maana kila kitu kipo wazi, utaratibu unajulika na mabadiliko ya Katiba nayo si jambo la mara moja hivyo taratibu zifuate na mengine yatafuata," alisema Kiganja.


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni