STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 31 Julai 2014

UJIO WA REAL MADRID TANZANIA, SASA RASMI FIGO NDANI YA NYUMBA



Wakati lisiti ya wachezaji wengine wa Real Madrid watakaokuja inasubiriwa kutajwa, sasa uhakika Luis Figo atakuwepo.

Kikosi cha wakongwe cha Real Madrid kinatarajia kucheza mechi ya kirafiki Agosti 23 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mechi hiyo itakuwa dhidi ya nyota wa Tanzania wakiwemo wale wanaocheza kikosi cha Taifa Stars, sasa.
Figo ni mmoja wa wachezaji wanaosubiriwa kwa hamu na mashabiki nchini.
Mratibu wa ziara hiyo, Ssebo amesema Figo ni kati ya wachezaji watakaokuwa na kikosi hicho jijini Dar.
“Kikosi chao ni kipana sana, kuna kina Owen, MacManamann, Zidane, Robertp Carlos na wengine wengi.
“Ila kuwapata wote inategemeana na majukumu fulani. Kama hawana majukumu yoyote, basi unaweza kuwapata wote.
“Sasa uhakika wa kumpata Figo upo kwa kuwa hatakuwa na majukumu wakati huo.
“Wengine pia watakuwa nyota wengi na tutaendelea kuwatangaza,” alisema Ssebo.
Mechi hiyo tayari imekuwa gumzo na Ssebo amewahakikishia mashabiki wa soka nchini kuwa kweli nyota hao watakuja nchini na wala si mzaha, hivyo wakae mkao wa kula.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox