Amerudi na mguu mbaya: Didier Drogba ameichezea tena kwa mara ya kwanza The Blues leo tangu arejee na imefungwa 3-0]
MKONGWE
Didier Drogba ameshindwa kung'ara akiichezea Chelsea kwa mara ya kwanza
tangu arejee msimu baada ya kuchapwa mabao 3-0 Werder Bremen nchini
Ujerumani katika mchezo wa kujiandaa na msimu.
Mshambuliaji
huyo wa Ivory Coast, aliichezea kwa mara ya mwisho Chelsea mwaka 2012
katika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, ikishinda kwa penalti dhidi ya
Bayern Munich, lakini jana akirejea Ujerumani yeye na washambuliaji
wengine wa The Blues- walilala kwa mabao ya Ludovic Obraniak kwa kichwa
na penalti za Assani Lukimya na Felix Kroos.
Kipa wa Chelsea, Thibaut Courtois amefungwa mabao mawili jana, wakati bao lingine alifungwa Petr Cech kipindi cha pili
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni