Mpiganaji mpya: Liverpool imetangaza kumsajili beki wa kulia wa Atletico Madrid, Javier Manquillo kwa mkopo
KLABU ya Liverpool imetangaza kumsajili beki wa kulia wa Atletico Madrid, Javier Manquillo kwa mkopo.
Beki
huyo wa kulia atakwenda kugombea namba na Glen Johnson katika jitihada
za kocha Brendan Rodgers kuendelea kuimarisha kikosi chake kwa ajili ya
msimu mpya.
Manquillo,
ambaye ana umri wa miaka 20 tu, alitemwa na Real Madrid akiwa na umri
wa miaka 14 tu, lakini tangu hapo amezichezea timu zote za taifa za
vijana za Hispania kuanzia chini ya umri wa miaka 16 hadi miaka 20.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni