STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatatu, 18 Agosti 2014

MANCHESTER UNITED YAWEKA MZIGO WA PAUNDI MILIONI 100 KUINASA SAINI YA ANGEL DI MARIA

Principal target: Manchester United are prepared to spend £100m on securing Angel Di Maria's signature
  Manchester United wanajiandaa kuwekeza kitita cha kutosha ili kuinasa saini ya Angel Di Maria kutoka Real Madrid.

MASHETANI wekundu, Manchester United wanajiandaa kumwaga paundi milioni 100 kumshawishi Angel di Maria kutua Old Trafford wakati huu klabu inahitaji kujiboresha ili kushindania ubingwa wa ligi kuu England.
Kocha mkuu wa United, Louis Van Gaal anahitaji kusajili wachezaji wa kiwango cha dunia kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili barani ulaya na tayari ameshaonja machungu ya kufungwa ambapo alilala mabao 2-1 dhidi ya Swansea jumamosi iliyopita uwanjani Old Trafford.
Mkurugenzi mkuu wa United, Ed Woodward amemuunga mkono Van Gaal na yupo tayari kufanya lolote lile ili mradi Di Maria atue Man United.
Inafahamika kuwa United imemuambia Muargentina huyo kwamba kwa kiwango chake cha sasa itamlipa mshahara wa paundi laki mbili kwa wiki.
Kwa mkataba wa miaka mitano anaotarajiwa kupewa, United itawezekeza paundi milioni 100 ikijumuisha mshahara wake na ada ya uhamisho.
Aware: Di Maria knows that Man United are willing to pay big bucks to bring him to Old Trafford this summer
 Di Maria anajua kuwa Man United wapo tayari kumlipa mkwanja mrefu ili atue Old Trafford.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox