MSHAMBULIAJI nyota wa
klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo, amemtabiria mafanikio mchezaji
mwenzake wa zamani Angel Di Maria katika klabu yake mpya ya Manchester
United.
Nyota huyo wa kimataifa wa argentina alifanikiwa kukamilisha
usajili uliovunja rekodi nchini Uingereza Jumanne iliyopita baada ya
kushindwa kufiti katika kikosi cha Carlo Ancelotti huku akipewa jezi
namba saba ambayo imewahi kutimiwa na Ronaldo wakati akiwa
United.
Ronaldo ambaye alicheza misimu sita na United, anaamini kuwa
uhamisho huo ndio Di Maria aliokuwa akihitaji na ana uhakika nyota huyo
anaweza kuisaidia timu hiyo kubadili mwelekeo baada ya kuanza vibaya
msimu mpya wa Ligi Kuu. Akihojiwa Ronaldo ambaye jana ametunukiwa tuzo
ya mchezaji bora wa mwaka barani Ulaya katika sherehe zilizofanyika
jijini Monaco, amesema Di Maria kwenda United ni jambo ambalo
litamsaidia kwani anaamini amekwenda katika moja ya klabu bora duniani
hivyo anamtakia mafanikio akiwa huko. Ronaldo aliendelea kudai kuwa
amezungumza naye na kumwambia kuwa jezi namba aliyopewa ina majukumu
makubwa lakini anadhani ataitendea haki jezi hiyo kwani ni mchezaji
mahiri.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni