STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumamosi, 16 Agosti 2014

SUAREZ: NI MUDA MUAFAKA WA KUSAHAU MAKOSA YANGU

Kazi imeanza: Luis Suarez akifanya mazoezi na wachezaji wenzake wa  Barcelona leo ijumaa akiwemo nahodha wa klabu, Xavi.

BAADA ya kuanza mazoezi na wachezaji wenzake wa Barcelona kwa mara ya kwanza jana ijumaa, Luis Suarez amesema ni muda wa kusahau miezi miwili iliyopita.
Siku ya Alhamis, mahakama ya juu ya rufani ya michezo ya CAS alitangaza kuwa kifungo cha miezi minne cha Luis Suarez kujihusisha na shughuli za michezo kisijumuishe na kutoshiriki mazoezi.
FIFA walimfungia Muuruguay huyo baada ya kumng’ata beki wa Italia, Giorgio Chiellin katika fainali za kombe la dunia-na hii ilikuwa mara ya tatu kukutwa na hatia ya kosa la aina hiyo.
Mshambuliaji huyo aliyejiunga na Barcelona akitokea Liverpool kwa dau la paundi milioni 75 alianza mazoezni na kikosi cha Barcelona ijumaa na anaweza kucheza mechi ya kwanza siku ya jumatatu katika mechi ya kirafiki dhidi ya Leon kwenye uwanja wa Camp Nou.
“Nina furaha kubwa ya kucheza tena mpira na wachezaji wenzangu,” Suarez aliiambia Tovuti ya Barca.
“Hali ya kutocheza ilinikosesha raha. Ninajutia makosa niliyoyafanya na niliomba msamaha, lakini haya yasahaulike”.

“Tufikirie ya baadaye katika klabu yangu ya Barcelona, klabu niliyoota kuichezea”.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox