Mbunge
wa Jimbo la Tabora Mjini, Ismail Aden Rage (CCM), ambaye pia ni Mjumbe wa Bunge
Maalum la Katiba, amenusurika kifo na kuumia bega la Kushoto akiwa na watu
wengine watatu baada ya gari alilokuwa akitumia kusafiria aina ya Toyota Lund
Cruser T 845 DQS (gari binafsi) kuacha njia na kuanguka katika eneo la
Chigongwe wakati akiwa njiani kuelekea mjini Dodoma kuanza vikao vya Bunge la
Katiba hapo kesho.
Kamanda
wa polisi mkoa wa Dodoma, David Misime, amesema ajali hiyo imetokea leo Agost
4, 2014 na kuwa imetokea katika eneo la Njia panda ya Kigwe katika barabara ya
Singida Dodoma, wakati mbunge huyo akielekea mkoani Dodoma kwa ajili ya kuanza
vikao vya Bunge Maalum la katiba.
Amesema
Rage, ameumia katika bega la kushoto na mgongoni huku Mbunge wa viti maalumu
mkoa wa Tabora, Munde Abdalla Tambwe, akiumia sehemu za kichwani na kuwa
majeruhi hao wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Dodoma.
Amesema
watu wengine waliokuwepo katika gari hilo ni pamoja na Mwanahamis Athumani,
John Hoya ambao wote kwa pamoja wanaendelea na matibabu katika hospitali hiyo.
Hata hivyo amesema chanzo cha ajali hiyo bado hakijafahamika, na kuwa polisi wanaendelea na uchunguzi ili kujua chanzo cha ajali hiyo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni