Mabingwa: Chelsea wakishangilia kombe la vijana chini ya miaka 21 kutoka timu za ligi kuu msimu wa 2013/14
MSIMU huu uongozi wa ligi kuu unatarajia
kuzindua mashindano mapya ya kombe la ulaya kwa timu za ligi kuu nchini
England chini ya miaka 21 na timu kutoka nje ya England.
Vikosi vya vijana chini ya miaka 21
kutoka timu nane (8) za juu katika msimamo wa ligi kuu Engalnd zikiwemo
klabu za Manchester City, Manchester United na Chelsea vitashiriki
pamoja na timu nane (8) kutoka nje ya England ambapo jumla ya timu
itakuwa ni 16.
Hii hatua ni kutekeleza mkakati maalumu
wa soka la vijana ulioanzishwa mwaka 2011 ili kuwaimarisha vijana
wanaozalishwa na klabu za juu za England.
Liverpool, walioshiriki ligi ya vijana
chini ya miaka 21 msimu uliopita hawatashiriki mashindano hayo na badala
yake nafasi hiyo imeenda kwa West Ham waliomaliza nafasi ya tisa katika
msimamo msimu uliopita.
Mashindano hayo yataenda sambamba na ligi ya vijana chini ya miaka 21.
Kwa sasa yatawavutia watu wengi zaidi kwasababu Sky Sports na BT Sports watarusha 'Laivu' mechi 10.
Waandaaji wana matumaini kuwa michuano
hii itawavutia watu wengi na timu zitapata wachezaji wao wazuri ili
kuwaingia katika timu za wakubwa.
Mkurugenzi wa akademi ya Schalke ,Oliver
Ruhnert alisaidia kuzalisha wachezaji wanne walioisadia Ujerumani
kutwaa kombe la dunia mwaka huu na timu yake itashiriki michuano hiyo ya
vijana chini ya miaka 21.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni