STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatatu, 25 Agosti 2014

UJERUMANI WANAWAKE NAO WANYAKUWA KOMBE LA DUNIA.

TIMU ya taifa ya wanawake ya Ujerumani imefanikiwa kunyakuwa Kombe la Dunia kwa wachezaji wanawake wenye umri chini ya miaka 20 kwenye michuano iliyokuwa inafanyika huko Montreal, Canada. 
 
Ujerumani walifanikiwa kuwazidi maarifa Nigeria katika mchezo wa fainali kwa kuwafunga bao 1-0 kama ilivyokuwa kwa timu ya wanaume iliyonyakuwa taji hilo katika michuano iliyofanyika nchini Brazil. 
 
Pamoja na kuonyesha mchezo mzuri huku wakimiliki vyema mpira, Nigeria walishindwa kabisa kupenya ngome ngumu ya wapinzania wao. Bao pekee katika mchezo huo lilifungwa na Lena Petermann ambaye alifunga katika dakika ya nane ya muda wa nyongeza baada ya timu hizo kushindwa kufungana katika muda wa kawaida. Mshambuliaji wa Nigeria na mfunmgaji bora wa mashindano hayo Asisat Oshoala alikosa nafasi kadhaa za wazi wakati golikipa wa Ujerumani Meike Kamper alitajwa kama mchezaji bora wa mechi hiyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox