MSHAMBULIAJI nyota wa
klabu ya Real Madrid Cristiano Ronaldo anaweza kuanza katika mchezo wa
ufunguzi wa La Liga dhidi ya timu iliyopanda daraja ya Cordoba pamoja na
kushambuliwa na majeruhi.
Nyota huyo wa kimataifa wa Ureno alitokea
benchi katika mchezo wa Super Cup uliochezwa Ijumaa iliyopita na
kufungwa na Atletico Madrid. Meneja wa Madrid Carlo Ancelotti amesema
Ronaldo amefanya mazoezi vyema hivyo anaweza kumpanga katika kikosi
chake.
Ancelottio alikiri kuwa wakati wa maandalizi ya msimu alikuwa
akisumbuliwa na majeruhi hivyo anahitaji kufanya jitihada ili aweze
kurejea katika kiwangop chake. Ronaldo mwenye umri wa miaka 29 ambaye
anashikilia tuzo ya mchezaji bora wa dunia alipata majeruhi ya mgongo
wakati timu hizo mbili zilipotoa sare ya bao 1-1 katika mchezo wa mkondo
wa kwanza.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni