STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatatu, 11 Agosti 2014

WACHEZAJI WATATU PEKEE WA UINGEREZA WAANZA KATIKA MCHEZO WA NGAO YA JAMII.


PAMOJA na mchezo kuchezwa katika Uwanja wa Wembley, nyumba ya soka la Uingereza ni wachezaji watatu pekee wa Uingereza walioanza katika mchezo wa Ngao ya Hisani kati ya Arsenal na Manchester City. Wachezaji wote watatu wa Uingereza waliocheza walikuwa ni wa Arsenal wakiwemo mabeki Kieran Gibbs na Calum Chambers na kiungo Jack Wilshere huku Alex Oxlade-Chamberlain akitokea benchi. 
 
Mabingwa wa Ligi Kuu Manchester City hawakuanzisha mchezaji hata mmoja wa Uingereza ambapo wote walianzia benchi akiwemo kipa Joe Hart, Micah Richards, James Milner na Scott Sinclair.
 
 Mwaka uliopita wachezaji 10 wa Uingereza walianza katika mchezo wa Ngao ya Jamii uliokutanisha timu za Manchester United na Wigan Athletic huku mwaka mmoja kabla ya huo wachezaji wanne pekee walianza katika mchezo kati ya Manchester City na Chelsea. 
 
Wadau mbalimbali wa soka nchini humo wamekuwa wakilalamika kutumika kwa wachezaji wa kigeni katika timu kubwa au Big Four akiwemo kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Uingereza Gary Neville. Neville amesema wamekuwa wakijimaliza taratibu kwani wamekuwa wakiwacheza Scotland na Jamhuri ya Ireland wakati wao wenyewe wanaelekea hukohuko. Neville aliendelea kudai kuwa miaka 25 iliyopita ilikuwa huwezi kukosa wachezaji kutoka Scotland au Jamhuri ya Ireland katika timu kubwa kama Liverpool na Manchester United lakini hivi sasa hakuna hata mmoja.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox