Daniel Agger akiwa na jezi ya Brondby baada ya kukamilisha uhamisho wake kutoka Liverpool
BEKI
Daniel Agger amerejea klabu yake ya zamani kwa mara ya kwanza tangu
mwaka 2006 baada ya Mdenmark huyokukamilisha uhamisho wa Pauni Milioni 3
kujiunga na Brondby.
Mlinzi
huyo wa kati anakwenda klabu hiyo ya Denmark kwa
Pauni Milioni 3 baada ya kupiga kazi Anfield kwa miaka nane.
Mwanasoka
huyo wa kimataifa wa Denmark amecheza jumla ya mechi 232 klabu hiyo ya
Merseyside, lakini ametwaa taji moja tu, Kombe la Ligi mwaka 2012,
maarufu kama Carling Cup Uwanja wa Wembley.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni