Di Maria amesema Real Madrid walimzuia kucheza Fainali Kombe la Dunia |
WINGA Angel di Maria amesema Real Madrid ilimuamrisha asicheze mechi ya Fainali Kombe la Dunia.
Mchezaji
huyo mpya wa Manchester United aliyesajiliwa kwa Pauni Milioni 60, dau
la rekodi kwenye soka ya Uingereza, tayari amemtupia lawama Rais wa Real
Madrid, Florentino Perez kwa kuondoka kwake kwa mabingwa hao wa Ulaya,
akisema hakuwa na nia ya kuondoka.
Di
Maria alikuwa shakani kuichezea Argentina katika Fainali ya Kombe la
Dunia dhidi ya Ujerumani Julai mwaka huu kwa sababu ya majeruhi, na
ameweka wazi kwamba uamuzi wa kutocheza mechi hiyo ulichukuliwa na
kocha Mkuu wa Argentina, Alejandro Sabella, na si Madrid ambao
walimtumia barua kumshauri asicheze."Nachopenda
zaidi ni kuichezea Argentina,"amesema Di Maria. "Nilipokea barua Saa
5:00 asubuhi kutoka Real Madrid, katika siku ya mchezo wakati nikiwa na
daktari wa viungo, akijaribu kufanya jitihada za kuniwezesha kucheza
fainali, ikiniambia nisicheze fainali ya Kombe la Dunia.
Nilikuwa
nafikiria kucheza fainali, na pia nilijua kwamba iwapo ningefanya hivyo
kulikuwa kuna asilimia 90 za kuumia tena. Nilipoisoma, nikaichana
barua. Nilipata maumivu sana asubuhi ile. Hicho ni kitu kibaya zaidi
kuwahi kunitokea maishani. Sikuzungumza na mtu yeyote katika klabu juu
ya hili. Haijalishi. Mwishowe, alikuwa ni Sabella aliyefanya maamuzi na
ilikuwa ni kwa nia nzuri," amesema.
Akizungumza
na kipindi cha Redio ya Argentina, America y Closs, Di Maria amesema:
"Nilizungumza na Alejandro na ulikuwa uamuzi wake. Sikutaka kumpa
shinikizo. Nilijua ningeweza kutoka née baada ya dakika 15 na kuiacha
timu, sikutaka hivyo," ameongeza.'
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni