Hatima ya Mshambuliaji wa Simba sc, Mganda Emmanuel Okwi (katikati) ni leo ama kesho
UONGOZI wa
Simba sc umepokea kwa furaha ushindi wa mabao 3-0 walioupata mbele ya mabingwa
wa Kenya, Gor Mahia ya Kenya katika mechi ya kimataifa ya kirafiki iliyopigwa
jioni ya jana katikauwanja waTaifa jijini Dar es salaam.
Mabao ya Simba yamefungwa na Paul Kiongera, aliyetia
kambani mawili na moja likizamishwa nyavuni na Ramadhan Singano ‘Messi’.
Makamu wa Rais wa Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’
mara baada ya kumalizika kwa mechi hiyo alisema wamefurahishwa na ushindi,
lakini kubwa zaidi ni namna timu ilivyocheza kwa kiwango cha juu.
“Kwa kweli tumepokea kwa furaha matokeo, lakini kubwa
sio ushindi peke yake bali ni jinsi gani timu imeweza kutandaza mpira chini”.
“Timu imecheza mpira maridhawa, imecheza
kitimu na kuwa na mipango ya kushambulia
na kutumia nafasi”. Alisema Kaburu.
“Kimsingi mambo haya kama uongozi yametufurahisha
na tunaamini timu itazidi kuimarika muda hadi muda kuelekea ligi kuu soka
Tanzania bara”.
Pia Kaburu alimzungumzia mshambuliaji wao Emmanuel
Okwi ambapo alisema nyota huyo alicheza mpira mzuri na kusababisha magoli
yaliyofungwa leo hii.
Kaburu aliongeza kuwa Simba haina tatizo na Yanga
bali Okwi ana matatizo na Yanga , lakini hapo kesho jibu litapatikana kutoka
kwa kamati ya sheria na hadhi ya wachezaji ya shirikisho la soka Tanzania.
Kiongozi huyo alisema Simba imepeleka majina
matano ya wachezaji wa Kigeni akiwemo Okwi, lakini beki wao Mkenya Donald
Mosoti hajajumuishwa licha ya kuwa na mkataba.
Kaburu alisema wanafanya taratibu za kumalizana na
Mosoti na wakati wowote ataondoka nchini.
Na kama Okwi hatapitishwa, Kaburu alisema Simba
ina wachezaji wengi wenye uwezo mkubwa wa kutandaza soka.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni