Nyota wa Mchezo: Angel di Maria alionesha kiwango cha hali ya juu.
Magoli matano kati ya sita yaliyofungwa
jana mjini Dusseldorf yalifungwa na wachezaji wanaocheza ligi kuu
England ambapo moja la Ujerumani lilifungwa na Andre Schurrle
anayekipiga Chelsea na lingine likatiwa kimiani na Gotze.
ANGEL di Maria alionesha uwezo wake wa
kutandaza kabumbu baada ya kutengeneza magoli matatu na kufunga moja,
Argentina akiwatandika 4-2 mabingwa wa dunia, Ujerumani.
Nyota huyo aliyevunja rekodi ya usajili ya Manchester United alitoa pasi za mwisho za magoli ya Sergio
Aguero, Erik Lamela na Federico Fernandez kabla ya kufunga la kwake
ikiwa ni kulipa kisasi cha kufungwa bao 1-0 katika fainali ya kombe la
dunia ambapo bao la dakika za nyongeza la Mario Gotze lilizima ndoto za
Argentina kutwaa kombe la dunia majira ya kiangazi mwaka huu nchini
Brazil.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni