Manchester United wameridhika na nyaraka za Radamel Falcao kuwa kweli ana umri wa miaka 28
MANCHESTER United wamejiridhisha kuwa nyota wao mpya, Mcolombia, Radamel Falcao hajadanganya umri wake.
Ripoti ziliibuka mwishoni mwa wiki kuwa Falco ana miaka 30 na sio 28.
Jambo hilo lilionekana kuteka hisia za
watu wengi kwasababu majira ya kiangazi mwakani United wana mpango wa
kumpa mkataba mrefu nyota huyo baada ya kumaliza mkataba wake wa mkopo
ulioigharimu paundi milioni 6.
Mkataba wanaotarajia kumpa Falcao utawafanya United wafikishe paundi milioni 52 katika usajili wa Mcolombia huyo.
Inafahamika kuwa United waliridhika na nyaraka zilizotolewa siku ya mwisho ya usajili juu ya mshambuliaji huyo.
Mwanzo mpya: Ripoti zinaeleza kuwa Falcao ana miaka 30, na sio 28, lakini United wanadai sio kweli
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni