BEKI
mpya wa Manchester United, Marcos Rojo anaweza kuichezea kwa mara ya
kwanza klabu yake hiyo katika mchezo wa Ligi Kuu ya England dhidi ya
Queens Park Rangers Uwanja wa Old Trafford Septemba 14 baada ya kupatiwa
hati ya kufanya kazi.
Rojo alisafiri hadi Lisbon Alhamisi ili kukamilisha taratibu za kupata hati hiyo ya kufanyia kazi England.
Kufanikiwa
kwa mchezaji huyo kupata hati hiyo ya kufanyia kazi ni faraja kwa kocha
Louis van Gaal, ambaye kikosi chake mina tatizo la safu ya ulinzi.
Taarifa ya Manchester United kwenye ukurasa wake wa Twiter
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni