Nyota
wa FC Barcelona, Luis Suarez akiwa ameshika jezi yake .
DIRISHA la usajili ni jambo muhimu
sana katika maisha ya wachezaji duniani. Wachezaji mbalimbali wanavuna
hela nyingi wakati wa usajili, lakini mpaka siku ya mwisho kuna baadhi
ya wachezaji wanashindwa kufikia ndoto zao.
Hapa chini ni orodha ya wachezaji waliouelezea usajili wa dirisha la majira ya kiangazi kwa namna ya kutimiza ndoto zao.
Marcos Rojo (Sporting Lisbon kwenda Man United): "Ilikuwa ndoto kucheza Manchester United. Ni ndoto kuwasili Manchester."
Mehdi Benatia (Roma kwenda Bayern Munich): "Bayern ina wachezaji wengi wakubwa. Wana kikosi imara na ni ndoto kuwa sehemu yao."
Chicharito (Man United kwenda Real Madrid): "Kwa upande wangu ndoto imekuwa kweli."
Danny Welbeck (Man United kwenda Arsenal): "Niliota kuichezea timu hii kabla. Kwangu mimi hatimaye imetokea."
Divock Origi (Lille
kwenda Liverpool): "Kwangu mimi ilikuwa ndoto kucheza klabu kubwa.
Najua Liverpool ni klabu yenye historia kubwa, kwahiyo kwangu mimi
imekamilika."
Dejan Lovren (Southampton kwenda Liverpool): "Ndoto imekuwa kweli."
Filipe Luis (Atletico
Madrid kwenda Chelsea): "nikiwa mtoto nilikuwa na ndoto ya kucheza ligi
kuu England siku moja, kwahiyo Chelsea walipokuja, kwangu mimi yalikuwa
maamuzi rahisi."
Matthias Ginter (SC Freiberg kwenda Borussia Dortmund): "Leo, nakamilisha ndoto yangu tangu nikiwa mtoto."
James Rodriguez (Monaco kwenda
Real Madrid): "Ni jambo la ajabu kusikia klabu kubwa kama Real Madrid
imevutiwa na mimi. Ilikuwa ndoto kusajiliwa na klabu ya ndoto zangu."
Luis Suarez (Liverpool kwenda Barcelona): "Siwezi kuamini kama ndoto nzuri kama hii imetimia."
Rickie Lambert (Southampton
kwenda Liverpool): "Siku zote nilikuwa na ndoto ya kuichezea Liverpool,
lakini nilidhani nafasi ya kuichezea imekwisha. Sikuwahi kuwaza kama
nafasi itarejea."
Ander Herrera (Athletic Bilbao kwenda Manchester United): "Kujiunga na Manchester United ni ndoto iliyokuwa kweli."
Ivan Rakitic (Sevilla kwenda Barcelona): "Ndoto imekuwa kweli."
Lakini inaonekana kwa wachezaji
fulani walikuwa na ndoto tofauti. Falcao alitweet kuwa ndoto ingetimia
kama angesajiliwa na Real Madrod badala yake alijiunga na Manchester
United ambapo alitangaza kama ndoto imekuwa kweli.
Nini tunajifunza hapa? ni kwamba
dirisha la usajili majira ya kiangazi limekamilisha ndoto za wachezaji
wengi walizokuwa nazo tangu utotoni.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni