Juan Zuniga alikumbatiwa na nahodha wa Brazil, Neymar kabla ya mechi ya kirafiki kuanza.
NYOTA wa Brazil, Neymar, ameonekana
kukubali msamaha wa Mcolombia, Juan Zuniga aliyemvunja mfupa wa uti wa
mgongo na kumaliza safari yake ya kucheza fainali za kombe la dunia
majira ya kiangazi mwaka huu katika ardhi ya nyumbani.
Neymar aliyeiongoza Brazil kwa mara ya
kwanza tangu achaguliwe kuwa nahodha na kocha wa timu ya Taifa, Dunga,
alimkumbatia Zuniga kabla ya kuanza mchezo ambao wazee wa Samba
walishinda 1-0 katika uwanja wa Sun Life mjini Miami.
Mshambuliaji huyo wa Barcelona alikosa
mechi zote zilizosalia za kombe la dunia katika ardhi yake kufuatia
kugongana na beki huyo wa Napoli, Zuniga wakati wa mechi ya robo
fainali.
Akionesha mapenzi: Neymar na Zuniga walikumbatiana katika uwanja wa Sun Life uliopo Florida, Miami
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni