Kiungo wa Juventus, Arturo Vidal amekunusha ripoti zinazodai ameumia tena.
KIUNGO wa Juventus, Arturo Vidal
amejibu mapigo kuhusu taarifa za kupata majeruhi tena kwenye goti lake
akiwa katika majukumu ya kimataifa na Chile.
Ripoti zilieleza kuwa Vidal, ambaye
alihusishwa kujiunga na Manchester United majira ya kiangazi mwaka huu,
aliondoka mazoezini mjini Miami baada ya kuumia goti kwa mara nyingine.
Mtu aliyewindwa: Kiungo wa Chile alihusishwa kujiunga na Manchester United wakati wa dirisha la usajili majira ya kiangazi.
"Goti langu liko sawa," Vidal aliandika
katika akaunti yake ya mtandao wa kijamii. "Tafadhali acheni kuzusha
taarifa. Njooni Chile".
Nyota huyo mwenye miaka 27 alifanyiwa
upasuaji wa goti mwishoni mwa msimu uliopita na alionekana kutokuwa fiti
sana katika fainali za kombe la dunia.
Majeruhi imemuathiri Vidal katika haraka zake za kujijenga kuwa miongoni mwa viungo bora wa dunia.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni