Mshambuliaji wa Arsenal,
Olivier Giroud anatarajia kupewa ofa ya kuongezewa mkataba mpaka majira
ya kiangazi mwaka 2018.
ARSENAL wamegeuzia macho yao katika
kuwatia kitanzi wachezaji waliopo katika kikosi chake baada ya kutumia
paundi milioni 80 katika usajili wa majira ya kiangazi mwaka huu.
Olivier Giroud na Mikel Arteta wote wapo
katika harakati za kuongezewa mikataba kufuatia klabu kusajili vipaji
vipya majira haya ya kiangazi akiwemo Alexis Sanchez na Danny Welbeck.
Taarifa zitakuwa nzuri kwa Giroud baada ya kuwa nje ya uwanja kwa miezi minne kutokana na kuvunjika kifundo cha mguu.
Naye kama kawa!: Mikel Arteta (kushoto) naye ataongezewa miezi 12 katika mkataba wake wa sasa Emirates
Majanga: Daktari wa viungo wa Arsenal, Colin Lewin akiingia uwanjani kumtibu Oliver Giroud baada ya kuumia kifundo cha mguu
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni