STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatatu, 8 Septemba 2014

YANGA SC WALIVYOYEYUSHWA NA DRFA, KUMBE BIG BULLETS WALIKAZIWA 0-0 NA EPAC UNITED LIGI YA MALAWI JANA! ANGALIA MATOKEO YA JANA LIGI HIYO

  Big Bullets waliodaiwa kuharibikiwa na gari wakija Tanzania kucheza na Yanga, jana jioni walitoka 0-0 dhidi ya EPAC United katika mchezo wa ligi kuu nchini Malawi.

YANGA SC jana ilitarajia kucheza mechi ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya Big Bulltes (zamani Bata Bullets) ya Malawi katika dimba la Taifa jijini Dar es salaam.
Mechi hiyo iliandaliwa na chama cha soka cha mkoa wa Dar es salaam, DRFA.
Jumamosi usiku baadhi ya viongozi wa Yanga na DRFA walikaririwa na baadhi ya vyombo vya habari wakisema Big Bullets wameshawasili nchini kwa usafiri wa barabara na walikuwepo Mbeya kuelekea Dar es salaam.
Saa 5 kabla ya mechi kuanza uwanja wa Taifa, Yanga walitangaza taafrifa za ghafla kwamba mechi hiyo haipo kwasababu Big Bullets hawajawasili nchini.
Ilielezwa gari walilokuwa wakisafiria Big Bullets liliharibika njiani kabla ya kuingia nchini.
Lakini kukawa na mkanganyiko, inawezekanaje timu iripotiwe kuwepo Mbeya tena na wahusika, halafu gari liharibike nje ya mpaka wa Tanzania. Kwa maana hiyo timu ilikuwa haijagusa mpaka wa Tanzania.
Niliwasikiliza viongozi wa DRF kwa umakini jana, kikubwa walichoeleza ni kwamba Big Bullets walipata matatizo na walikuwa na mawasiliano ya karibu sana mpaka usiku ‘mkubwa’ wa jumamosi.
DRFA wanasema jitihada za kutengeneza gari la timu hiyo ziligonga mwamba na ndipo wakachukua maamuzi ya kuahirisha mechi na jitihada za kutafuta timu nyingine ziligonga mwamba.
Pia waliwaomba radhi mashabiki kwa usumbufu uliojitokeza. Kwa upande wa Yanga, hawakuwa tayari kuelezea kilichotokea zaidi ya kusema DRFA waulizwe.
Walikuwa sahihi kujibu hivyo kwasababu DRFA ndio walikuwa waandaji, lakini hawakwepi lawama ya kuwaangusha mashabiki wao kwasababu walishindwa kufuatilia kwa ukaribu zaidi taarifa za ujio wa timu hiyo.
Kuahirishwa kwa mechi hiyo kulileta usumbufu mkubwa kwa mashabiki hasa waliotoka nje ya Dar es salaam.
Wengine walipata taarifa wakiwa njiani kwenye mabasi, wakati wengine hawakupata kabisa mpaka walipofika uwanjani na kukuta hakuna dalili ya mechi.
DRFA walifanya makosa juu ya hili, ingawa sipingani na kuwepo kwa sababu zilizo nje ya uwezo kama gari kuharibika.
Lakini mwisho wa yote, jana usiku iliripotiwa kuwa timu ya Big Bullets jana jioni ilikuwa na mchezo wa ligi kuu nchini Malawi (TNM) dhidi ya EPAC United, uwanja wa Kamuzu mjini Blantyre.
Mchezo huo mkali na wa kusisimua ulimazika kwa suluhu ya bila kufungana.
Kwa matokeo ya jana, Big Bullets walifikisha pointi 36 katika nafasi ya pili baada ya kucheza mechi 17, sawa na vinara Moyale Barracks ambao wanaongoza kwa wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Timu iliyokuwa na mechi ya ligi nchini Malawi, pia ilikuwa njia kuja Tanzania, lakini iliharibikiwa na gari njiani. Ni Big Bullets hii ninayoifahamu au kuna nyingine?
Labda walituma kikosi cha pili cha Big Bullets kuja kucheza Tanzania, lakini mbona DRFA hawakueleza hivyo?
Matokeo ya ligi ya Malawi wikiendi (jumamosi na jumapili) iliyopita kwa mujibu wa Mtandao wa SOCCERWAY.
Sat
06/09/14










Sun
07/09/14









3: 0


Kwa sasa dunia imebadilika, si rahisi tena kudanganya kama zamani.
Wakati ambao mtu mwenye uwezo alikuwa anaweza kuona kitu kwenye TV halafu akawaambia wasio na TV kuwa nimeota itakuwa hivi.
Kila kitu kipo wazi, Napata shida kujua kama kweli DRFA walikuwa na mawasiliano na Big Bullets.
Kama ndio hii iliyocheza ligi kuu nchini Malawi, basi tuna safari ndefu katika utawala wa mpira wa mpira wa miguu.

Labda DRFA watakuja kutolea ufafanuzi zaidi ya taarifa yao ya jana.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox